STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Friday, July 5, 2013

Christian Bella jukwaani tena na Diamond Musica

Christian Bella
BAADA ya kufanya onyesho lao kwa kishindo, mwimbaji Christian Bella atashiriki tena onyesho la pili leo na bendi ya Diamond Musica Original ikiwa ni mwendelezo wa mikakati ya kujiandaa kumchukua ili ajiunge na bendi hiyo inayokuja kwa kasi.
Onyesho la kwanza kati na mwimbaji huyo na bendi ya Diamond Musica Original lilifanyika Ijumaa iliyopita na kupata mashabiki wengi waliojitokeza kulishuhudia na sasa limeandaliwa jingine litakalofanyika leo na huenda likamshirikisha pia Ndanda Kosovo.
Kwa mujibu wa mkurugenzi wa bendi hiyo, Ally Ocs, maonyesho hayo yanalenga kumkaribisha Bella na kisha uongozi wa bendi utafanya naye mazungumzo ili kuona uwezekano wa kumchukua jumla mwimbaji huyo.
"Kama nilivyowahi kusema siku za nyuma Ndanda Kosovo tulishamchukua na huenda akawapo kwenye onyesho letu kwani wakati wowote anatarajia kurejea kutoka kwao Kongo alikokwenda kusalimia kabla ya kuanza kazi rasmi katika bendi yetu," alisema Ocs.
Mkurugenzi huyo alisema kuwa katika onyesho atatambulishwa pia mnenguaji Mariam Bessie aliyechukuliwa kutoka bendi ya Mapacha Watatu inayoongzwa na Khalid Chokoraa na Jose Mara.
"Tumedhamiria kuingia kwenye muziki wa ushindani, hivyo hatuna budi kujipanga kisawasawa na hilo litawezekana kwani hadi sasa mambo yetu yanakwenda vizuri ikiwa ni pamoja na kuwachukua wanamuziki wenye majina makubwa," alisema.
Diamond Musica Original iko kwenye maandalizi ya albamu ya kwanza ikiwa imekamilisha baadhi ya nyimbo kama: 'Hatua',  'Shilingi', 'Upole wa Mapenzi', 'Fimbo la Mwaka', 'Kibali cha Mapenzi' na 'Deceiption'.

No comments:

Post a Comment