STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Friday, July 5, 2013

Saida Karoli kutambulisha mpya Igunga, Nzega

Saida Karoli
MSANII nyota wa muziki wa asili, Saida Karoli ambaye alivumishiwa kifo hivi karibuni anatarajiwa kujitokeza hadharani kwa mara ya kwanza kufanya maonyesho maalum ya kudumisha amani yatakayofanyika mkoani Tabora.
Karoli aliyewahi kutamba na nyimbo mbalimbali kama 'Chambua kama Karanga' na nyingine atafanya onyesho la kwanza siku ya Jumapili katika shamrashamra za kusherehekea sikukuu ya Sabasaba mjini Igunga na kutambulisha nyimbo zake mpya kwa mashabiki wa mji huo.
Kwa mujibu wa mratibu wa maonyesho hayo, Livenus Madaraka, onyesho la pili la mwanadada huyo litafanyika Julai 9 katika mji wa Nzega, akiwadhihirishia mashabiki wake kwamba yu hai na anaendeleza 'makamuzi' kama kawaida.
Mratibu huyo alisema amewataka wale ambao bado hawajaamini kama Saida Karoli anadunda wajitokeze katika maonyesho hayo ambapo msanii huyo ameahidi kufanya makubwa katika kuwapa burudani mwanzo mwisho.
"Mwenyewe ameahidi kukata kiu ya mashabiki wake kwa kuwapa burudani kabambe na kuzitambulisha nyimbo zake mpya na zile za zamani zilizompatia umaarufu mkubwa ndani na nje ya Tanzania," alisema Madaraka.

No comments:

Post a Comment