STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Friday, July 5, 2013

Tamasha la Matumaini kurindima Jumapili

 http://api.ning.com/files/X378Xfy1meuzEX8xHlBh-qQB8hV-1a9IRTU-sWUlJ2vVfLOTpjokDf51r7zq*IPOR8Llw33BkDDIl5dVaYmxQm*gckOwOa6v/ngumi.jpg
WANAMICHEZO, wanamuziki, wasanii wa filamu na wabunge wamezidi kutambiana kuelekea Tamasha la Usiku wa Matumaini litakalofanyika keshokutwa kwenye Uwanja wa Taifa jijini Dar es Salaam kuchangia mfuko wa elimu nchini.
Wakizungumza na waandishi wa habari jijini Dar es Salaam jana, baadhi ya washiriki wa tamasha hilo walisema wamejiandaa vyema huku kila upande ukitamba kufanya vizuri.
Mbunge wa Kinondoni, Idd Azzan, ambaye pia ni kipa wa timu ya wabunge alisema kikosi chao kinachoendelea na mazoezi jijini Dar es Salaam kiko vizuri na wana ukakika wa kuendelea kuifunga Yanga kama walivyoifunga mwaka jana.
Mratibu wa tamasha hilo, Abdallah Mrisho alisema kutakuwa pia na burudani kutoka kwa bendi za DDC Mlimani Park na Msondo, taarab ya Mzee Yusuf na muziki wa kizazi kipya kutoka kwa Diamond Platinumz, Chege, H.Baba na Mkenya Prezzo.
"Pia kutakuwa na muziki wa injili kutoka kwa wasanii Upendo Nkone, Solomon Mukubwa, Anastazia Mukabwa, Flora Mbasha na Asha Mwaipaja wa Mbeya," alisema Mrisho.
Mbali na wabunge wa Simba na Yanga kuvaana katika soka, pia kutakuwa na mechi nyingine kati ya wasanii wa Bongo Movie dhidi ya Bongo Fleva na mapambano ya ngumi kati ya mbunge Zitto Kabwe na Vicent Kigosi (Ray), Jacqueline Wolper dhidi ya mbunge Halima Mdee na Aunt Ezekiel dhidi ya mbunge Ester Bulaya.

No comments:

Post a Comment