STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Sunday, July 28, 2013

Lion Boy amtwanga Mthailand kwa KO

Omari Kimweri
BONDIA Mtanzania Omari Kimweri  'Lion Boy' anayefanya shughuli zake nchini  Australia ameendelea kutamba katika nchi hiyo baada ya jana kumtwanga kwa  KO ya raundi ya kwanza bondia Ekkalak Saenchan wa Thailand   ikiwa ni mchezo wake wa 16 tangu aingie katika ngumi za kulipwa nchini humo 
Bondia huyo ambaye anaitangaza vyema nchi ya Tanzania Kimataifa ameahidi kuenderea kutoa vipigo kwa mabondia  mbalimbali  pindi wakutanapo ulingoni 
Bondia huyo aliyezaliwa Tanzania katika jiji la Dar es salaam mwaka1982 amekuwa gumzo nchini humo kwa kuonesha mchezo mzuri unaowavutia raia wengi wa Australia na kuweza kuwa bondia namba moja katika nchi hiyo huku katika Dunia akishikilia nafasi ya 52 katika mabondia 450 duniani wenye uzito wa light flyweight

Anasema lengo lake kubwa ni kuukamata ubingwa unaotambulika kimataifa Duniani wa WBA World light flyweight title unaoshikiliwa na bingwa namba moja Duniani ,Roman Gonzalez na IBF light flyweight title   unaoshikiliwa na  John Riel Casimero wa  Philippines ambao wanamuumiza kichwa.

No comments:

Post a Comment