STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Thursday, August 1, 2013

Azam kutimkia Bondeni kucheza mechi nne ratiiba kamili hii hapa!

Azam FC  inasafiri jumamosi hii kuelekea afrika ya kusini kwa maandalizi ya ligi kuu na itacheza michezo minne kama ifuatavyo
Tarehe 5 August, Azam Fc vs Kaizer Chiefs, 
Tarehe 7 August Azam Fc vs Mamelodi Sundows, 
Tarehe 9 August Azam Fc vs Orlando Pirates,
Tarehe 12 August Azam Fc vs Moroka Swalows
Kikosi cha Azam
KLABU ya soka ya Azam Fc, inatarajiwa kuondoka nchini keshokutwa kwenda Afriki Kusini kuweka kambi yao kujiandaa na msimu mpya wa Ligi Kuu Tanzania Bara 2013-2014.
Kwa mujibu wa taarifa za klabu hiyo timu hiyo ikiwa nchini humo itacheza mechi nne kabla ya kurejea nchini kuisubiri Yanga katika pambano la Ngao ya Hisani Agosti 17 na kisha kuifuata Mtibwa Manungu katika pambano la fungua dimba la Ligi Kuu.
Ratiba hiyo iliyotolewa na klabu hiyo inaonyesha itashuka dimbani Agosti 5 dhidi ya Kaizer Chiefs kabla ya siku moja baadaye kuwava Mamelodi Sundowns.
Baada ya siku moja yaani Agosti 9 Azam itaumana na Orlando Pirates na kumalizia ziara na kambi yao ya nchini humo kwa kuvaana na Moroka Swallows Agosti 12.

No comments:

Post a Comment