STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Thursday, August 1, 2013

Maajabu ya Dunia! wanandoa waliozaliwa siku moja wafa siku moja wakiwa na miaka 94

WANANDOA katika jijini la California waliozaliwa siku moja na kuoana miaka 75 iliyopita wamefariki siku moja wakiwa na miaka 94.
 Couple Born on Same Day, Married 75 Years, Die One Day Apart

Kwa mujibu wa Taarifa iliyotolewa na Long Beach Press Telegram, Helen na Les Brown walifariki Julai 16 na 17 mwaka huu wote wakiwa na umri wa miaka 94.

Zach Henderson, Mmilikii wa Grosari moja ijulikanayo kwa jina la Ma N’Pa iliyopo Long Beach alinukuriwa wakisema kuwa alikuwa akiwaona wapendanao hao kila siku iitwayo kwa Mungu na kuuita uhusiano wao kuwa “ a Wonderful Blessing”.

Kwa mujibu wa taarifa iliyotolewa na Press –Telegram imesema kuwa wote walizaliwa siku moja yaani Desemba 31, 1918 na pia walianza kuwa pamoja mwaka 1937 katika masomo ya sekondari.

Imejulikana kwamba wanandoa hao walikuwa waamini wa Mashahidi wa Yehova (Jehova Witnesses) waliobarikiwa kuwa na mtoto wao Les Brown Jr.

Henderson anasema imani yao kwa Mwenyezi Mungu ndio iliyozidi kuimarisha ndoa yao hadi kufikia hapo.

Mtoto wao Les Brown Jr alinukuriwa akisema “Walikuwa pamoja kila siku kwa miaka 75, hakika upendo wao ulirandana” 

Post Telegram limeripoti kuwa Les Brown alikuwa akiumwa ugonjwa wa Parkison’s na mkewe Helen Brown alikuwa akisumbuliwa Kansa ya tumbo hadi mauti yao yalipowakuta

"She was completely cognitive," Henderson said, describing how he found Helen Brown a few days before she died. "It seems like she was waiting for Les to be comfortable and they were going to move on to something else with each other."

Ibada ya pamoja itafanyika siku ya Jumamosi mchana kwa ajili ya kuwakumbuka wanandoa hao huko Long Beach, California.

CHANZO: JAIZMELALEO/ABC NEWS/YAHOO NEWS

No comments:

Post a Comment