STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Tuesday, August 20, 2013

Haya ndiyo mashtaka yanayomkabili Sheikh Ponda Issa Ponda

Sheikh Ponda akiwasili mahakamani
Ulinzi wa kufa mtu!
Tuktuk alilosafirishiwa Sheikh Ponda

Sheikh Ponda akishuka kwenye gari
Sheikh Ponda akiwa kizimbani
 
KIONGOZI wa Jumuiya na Taasisi za Kiislamu Tanzania, Sheikh Issa Ponda jana alipandishwa kizimbani katika Mahakama ya Hakimu Mkazi Mfawidhi mkoa wa Morogoro kujibu mashitaka matatu yanayomkabili.
Mashtaka yaliyofunguliwa dhidi ya kiongozi huyo wa umma wa Kiislam ni kutotii amri halali, kutoa maneno yenye nia ya kuharibu imani za dini na kushawishi  kutenda kosa. 
 

Sheikh Ponda amefikishwa mjini Morogoro na helkopta ya jeshi la polisi majira ya saa tano asubuhi  chini ya ulinzi mkali ambapo askari waliimarisha ulinzi kwa muda wote huku kikosi cha kutuliza ghasia FFU wakiwa na silaha mabomu na mbwa ambapo hali hiyo imesababisha kusimama kwa baadhi ya shughuli zingine za kiofisi katika ofisi zilizopo jirani na mahakama ya hakimu mkazi wakati kesi hiyo ikiendelea.

Akisoma shataka mbele ya hakimu mkazi Richard Kabate , wakili mkuu wa serikali kanda ya Morogoro Benard  Kongola amedai kuwa shekh Ponda anadaiwa kutenda makosa hayo matatu Agosti 10 mwaka huu majira ya jioni katika viwanja vya Shule ya Msingi Kiwanja cha Ndege, mjini Morogoro.

Katika shitaka la kwanza la shekhe Ponda anadaiwa kutotii amri halali ambapo shitaka la pili anadaiwa kutoa maneno yenye nia ya kuharibu imani za dini kwa kutoa maneno kuwa serikali iliamua kupeleka jeshi  Mtwara kushughulikia suala la vurugu iliyotokana na gesi kwa kuwaua na kuwatesa wananchi kwa sababu asilimia 90 ya wakazi wa Mtwara ni Waislamu. 


Shitaka la tatu linalomkabili shekh Ponda ni kushawishi na kutenda kosa ambapo anadaiwa kuwa alitoa maneno ya ushawishi kwa kuwataka  waislaam wasikubali uundwaji wa kamati za ulinzi na usalama za misikiti kwani zinaundwa na Bakwata ambao ni vibaraka wa CCM na serikali, na kama kamati hizo zitajitokeza aliwaamuru wafunge milango na madirisha ya misikiti kuwapiga.  Upande wa mashitaka umedai kuwa upelelezi umekamilika na kesi hiyo itasomwa tena Agosti 28  mwaka huu ambapo mstakiwa amerudishwa rumande kwa helkopta jijini Dar es salaam.

Baada ya kusomewa mashitaka hayo Sheikh Ponda anayetetewa na mawakili wasomi Barthoromew Tarimo na Ignas Punge  alikataa mashataka yote matatu na hivyo upande wa mashitaka kupinga dhamana kwa madai kuwa sheikh Ponda anatumikia kifungo cha nje na kwamba hakutakiwa kufanya kosa, hata hivyo anakabiliwa na makosa mengine.
 

No comments:

Post a Comment