STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Tuesday, August 20, 2013

Nyilawila atimka Russia, kuzipiga Jumamosi nchini humo

BONDIA mchachari wa ngumi za kulipwa nchini, Karama Nyilawila 'Captain' ameondoka nchini kwenda Russia kwa ajili ya pambano lake la kimataifa dhidi ya mwenyeji wake, Fedor Chudinov atakayepigana naye siku ya Jumamosi (Agosti 24, 2013).
Nyilawila aliyepitia nchini Kenya kwa ajili ya kuungana na wakala wake, Franklyn Imbenzi kwa ajili ya kuelekea Russia, atapanda ulingoni kupigana na Chudinov katika pambano l;a uzito wa kati la raundi nane litakalochezwa kwenye mji wa Vulgo Grad.
Kwa mujibu wa taarifa iliyotolewa na Oganaizesheni ya Ngumi za Kulipwa Tanzania (TPBO-Limited), ambayo ndiyo iliyotoa kibali kwa Nyilawila kwenda Russia, bondia huyo aliondoka juzi Jumapili kupitia Nairobi Kenya kabla ya kuelekea Urusi kwenye pambano hilo.
Hilo litakuwa pambano la kwanza la kimataifa kwa Nyilawila, tangu 2010 alipomtwanga Kreshnik Qato wa Albania  na kutwaa taji la kimataifa la WBF ambalo alikuja kuvuliwa baada ya kugoma kwenda kulitetea ili apigane kirafiki na Francis Cheka  mwaka 2012.
TPBO-Limited, limemtakia kila la heri bondia Nyilawila ili apeperushe vyema bendera ya taifa kwa kufanya vizuri katika pambano hilo la kimataifa litakalomrejesha tena kwenye ramani ya mchezo huo.

No comments:

Post a Comment