Nyilawila aliyepitia nchini Kenya kwa ajili ya kuungana na wakala wake, Franklyn Imbenzi kwa ajili ya kuelekea Russia, atapanda ulingoni kupigana na Chudinov katika pambano l;a uzito wa kati la raundi nane litakalochezwa kwenye mji wa Vulgo Grad.
Kwa mujibu wa taarifa iliyotolewa na Oganaizesheni ya Ngumi za Kulipwa Tanzania (TPBO-Limited), ambayo ndiyo iliyotoa kibali kwa Nyilawila kwenda Russia, bondia huyo aliondoka juzi Jumapili kupitia Nairobi Kenya kabla ya kuelekea Urusi kwenye pambano hilo.
Hilo litakuwa pambano la kwanza la kimataifa kwa Nyilawila, tangu 2010 alipomtwanga Kreshnik Qato wa Albania na kutwaa taji la kimataifa la WBF ambalo alikuja kuvuliwa baada ya kugoma kwenda kulitetea ili apigane kirafiki na Francis Cheka mwaka 2012.
TPBO-Limited, limemtakia kila la heri bondia Nyilawila ili apeperushe vyema bendera ya taifa kwa kufanya vizuri katika pambano hilo la kimataifa litakalomrejesha tena kwenye ramani ya mchezo huo.
No comments:
Post a Comment