STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Tuesday, August 20, 2013

Bibi Cheka sasa alia videoni

https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEgb4ddGFF-_jlkI6BjyvEoPbRlZI_PsxKeFVhZEecs4BlpZTswOKt4y3CxqQb7mIcLdbNwj82vP9W7Yp5dJBtOeuEQ_P5nE9EgHXH8UdsNyIxj_qvdPU-STM0-5V9K7qnSWAC3KOMdlGB4u/s640/bi+chekaaaa.jpg
Bibi Cheka
BAADA ya nyimbo zake za 'Ni Wewe' na 'Good Baba Fella' kufanya vyema, msanii mwenye umri mkubwa lakini chipukizi katika muziki wa kizazi kipya nchini, Cheka Hija 'Bibi Cheka' amekamilisha video ya wimbo mpya uitwao 'Nalia' inatarajiwa kuanza kusambazwa wiki hii.
Meneja wa msanii huyo, Said Fella aliiambia MICHARAZO asubuhi hii kuwa, video hiyo iliyorekodiwa na kampuni ya Fast Door na itaanza kutolewa kabla ya 'audio' yake tofauti na nyimbo za nyuma.
Fella alisema wameamua kutanguliza video kabla ya 'audio' katika kuleta tofauti na kazi za awali za mkongwe huyo aliyewahi kuwa mnenguaji wa bendi ya Msondo Ngoma enzi iitwa JUWATA.
"Baada ya kimya tangu alipotoa 'Good Baba Fella', Bibi Cheka amefyatua kazi mpya akiakamilisha video ya wimbo wake wa tatu uitwao 'Nalia' itakayoachiwa wiki hii, wakati 'audio' ikifuata baadaye," alisema.
Fella alisema tofauti na nyimbo za awali zilizomtambulishwa msanii huyo mwenye ambapo aliimba kwa kushirikiana na wasanii wengine, safari hii Bibi Cheka kauimba 'Nalia' peke yake.
Katika wimbo wake wa kwanza wa 'Ni Wewe', mkongwe huyo alimshirikisha Mheshimiwa Temba na aliimba na Godzillah katia kibao cha 'Good Baba Fella'.
Mbali na nyimbo hizo zake binafsi, Bibi Cheka mwenye umri zaidi ya miaka 50 alishirikishwa pia katika nyimbo kadhaa za wasanii wa TMK Wanaume Family, ukiwamo 'Mario' wa Mhe Temba.

No comments:

Post a Comment