STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Tuesday, August 6, 2013

Rufaa 84 zakatwa Baraza la Ushidani

http://www.fullshangweblog.com/wp-content/uploads/2013/08/IMG_1843.jpg
Na Suleiman Msuya
KWA kipindi cha zaidi ya miaka sita tangu kuanzishwa kwa Baraza la Ushindani (FCT) jumla ya rufaa 84 zimesajiliwa 36 zimesikilizwa na kutolewa uamuzi na jopo la wajumbe waa Baraza hilo.
Hayo yamebainishwa Mkuu wa Kitengo cha Masuala ya Uchumi wa FCT Nzinyangwa Mchany wakati akijibu swali la mwandishi wqa habari hii leo jijini Dar es Salaam.
Alisema katika rufaa hizo 29 zilisitishwa kutokana na wahusika kuamua kuziondoa baada ya kufikia maamuzi ambayo baraza hilo halina mamlaka yakuingilia ambapo kwa sasa rufaa zinazoendelea kusikilizwa ni 19.
Mchany alisema Baraza la Ushindani limejipangia kusikiliza rufaa 24 kwa mwaka iwapo zitakuwepo lakini bado mwitikio ni mdogo hali ambayo inatajwa kuwa inachangiwa na uelewa mdogo kutoka katika jamii juu ya FCT.
“Baraza la Ushindani FCT limeanza kazi rasmi mwaka 2007 ambapo huwa tunapokea rufaa kutoka katika kwa watu na taasisi mbalimbali ambazo zinakuwa hazijaridhika na maamuzi ambayo yanatolewa na  mamlaka za udhibiti hapa nchini,” alisema.
Kwa upande wake Mwanasheria Mwandamizi Hafsa Said  alisema pamoja na mafanikio hayo madogo ambayo wameweza kuyapata tangu kuanza kwa FCT bado wana changamoto chache ambazo zinawakabili.
Alizitaja baadhi ya changamoto kuwa ni uchache wa majaji wa kusikiliza rufaa ambapo wamekuwa wakifanya kazi kwa muda maalumu (party time) kutokana na ukweli kuwa ni watumishi wa Mahakama ya Kuu nay a Rufaa.
Said alitaja changamoto nyingine ni ufahamu mdogo kwa jamii juu ya FCT ambapo wanajipanga kwa kushirikiana na mamlaka za udhibiti kutoa elimu hiyo ili wananchi na jamii kwa ujumla kutopoteza haki zao pale wanapoona kuna dalili za kuzikosa.
Pia alisema pamoja na changamoto hizo kupitia maamuzi yao wanayotoa ubora wa mamlaka za udhibiti umeongezeka jambo ambalo linaleta tija kwa jamii.
Alisema tangu waanze kupokea rufaa zinazotoka kwa taasisi na watu binafsi asilimia kubwa ya maamuzi yamekubalika ambapo ni maamuzi mawili tu ndio yaliendelea katika ngazi zingine za kimaamuzi.
Mwanasheria huyo Mwandamizi alitoa wito kwa wananchi na taasisi mbalimbali ambazo zinasimamiwa na mamlaka kama TCRA, SUMATRA, EWURA, FCC na TCAA kujitokeza kukata rufaa iwapo watakuwa hawajaridhika na maamuzi yao.

No comments:

Post a Comment