STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Friday, September 6, 2013

Afande Sele kuzindua Novemba

Afande Sele

MSANII mkongwe wa muziki wa kizazi kipya, Seleman Msindi 'Afande Sele' anatarajia kufanya uzinduzi wa albamu yake mpya iitwayo 'Kingdom wa Amani na Upendo' utakaofanyika Novemba mwaka huu mjini Morogoro na kusindikizwa a  wasanii mbalimbali nyota wa hapa nchini.
Akizungumza na MICHARAZO Afande Sele, alisema kwa sasa ni mapema kuwataja wasanii watakaomsindikiza kwa sababu anaendelea kumalizana na wadhamini wake.
Alisema kwa sasa anajipanga kuitambulisha albamu hiyo kwa kuachia video ya wimbo unaoendelea kutamba wa 'Dini Tumeletewa' alioimba kwa kushirikiana na Belle 9.
Mkongwe huyo alisema albamu hiyo itakuwa na nyimbo 10 na siku za uzinduzi itaachiwa 'audio' na video yake kwa mpigo ili mashabiki wake wapate vitu kamili kwa wakati  mmoja.
Alitaja baadhi ya nyimbo za albamu hiyo ni pamoja na 'Dini Tumelewa', 'Amani na Upendo', 'Soma Ule', 'Mi Sielewi', 'Karibu Moro', 'Sukari na Chai', 'Simba Dume na 'Kingdom'.

No comments:

Post a Comment