STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Friday, September 6, 2013

Fundi Kinyambe fumbafu thana

Kinyambe (kushoto) akiwa na Mzee Jangala

MCHEKESHAJI mahiri nchini James Mohammed 'Kinyambe'  amefyatua filamu tatu binafsi ambazo amepanga kuziachia moja baada ya nyingine hivi karibuni.
Kinyambe anayetamba kwenye kipindi cha vichekesho cha 'Vituko Show' alizitaja filamu hizo kuwa ni 'Fundi Kinyambe', The Twins na ' Fumbafu Thana' kuanzia Novemba mwaka huu.
Akizungumza na MICHARAZO, Kinyambe alisema filamu hizo amepanga kuziachia moja moja kuanzia Novemba mwaka huu.
Kinyambe alisema filamu hizo za vyumba mbavu ameigiza na wasanii mbalimbali nchini wakiwamo wenzake wanaoigiza nao katika kipindi cha 'Vituko Show'.
"Ni kati ya kazi zinavyomfanya mtazamaji ashikilie mbavu zake mwanzo mwisho, nitaanza kuziachia rasmi Novemba nikianza na 'Fundi Kinyambe' kisha 'The Twins' na kumalizia 'Fumbafu Thana'," alisema Kinyambe.

No comments:

Post a Comment