STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Friday, September 6, 2013

Mhe. Ndugai atupiwa lawama vurugu za jana bungeni

https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEgbR2CeEeeh8aIgUAxVg23rr5e1DG0s7zx41yhCH6ZY0ziYoTLNSlZ-GP5_9Ea0yd37vWfoS1hBkiDketxjf3x7RCdF75YebSxZRnTJ2pZrrF6f6fURo2Bm3aA0BXX6bHz5R5_eUhGDKMDI/s400/_MG_0724+MBILI.JPG

Wanabodi, 
Mwaka mmoja uliopita niliwahi kuleta hoja hii humu Wito: Wabunge Badilini Kanuni Kuondoa Udikteta wa Spika/N.Spika!
Leo nimeikumbuka kufuatia vurugu za jana bungeni!.
Chanzo cha vurugu zile ni "Ukosefu wa Busara Ndogo Tuu toka kwa Naibu Spika!".
Tangu tumepata uhuru, Tanzania imekuwa nchi ya chama kimoja kwa kipindi kirefu, tulipoingia mfumo wa vyama vingi ile 1992, tulifanya marekebisho tuu ya kanuni, ila hatukuweza kufanya mabadiliko ya "mind set" toka mfumo wa chama kimoja hadi mfumo wa vyama vingi, hivyo hali hii imeendelea mpaka sasa kwa CCM ambayo ndio chama tawala, kuendelea kuonekana ni chama dola kwa sababu ndiyo inayoongoza dola, na nafasi ya vyama vya upinzani kuonekana vipo vipo tuu kwa vile vimeanzishwa kwa mujibu wa sheria!.
Kufuatia hali hii ya "CCM Supremacy" kunapelekea viongozi wa mihimili mikuu ya nchi, Bunge, Mahakama na Serikali, kutimiza wajibu wake kwa mlengo wa heshima kwa CCM kwa sababu M/Kiti wa chama tawala ndie head of Executive, ambaye ndiye rais wa nchi anaeteua kila mtu!.
Huku kujikomba komba kwa CCM, kumepelekea hata Spika na Naibu Spika ambao walipaswa kutimiza majukumu yao independently, wanajikuta wakiifavour CCM, kwa lengo la kujikomba komba huku wakiliangamiza taifa bila wao kujijua kwa kisingizio kuwa kwa vile CCM ndio chama tawala!.
Kwa mujibu wa uendeshaji wa mabunge ya vyama vingi, Mkuu wa shughuli za serikali bungeni, ambaye ni Waziri Mkuu, na Kiongozi wa Upinzani Bungeni, KUB, ambaye ni Mhe. Freeman Mbowe, wana hadhi sawa kabisa ndani ya bunge!. Hakuna mmoja ambaye ni mkubwa zaidi ya mwingine wala hakuna aliyebora zaidi ya mwenzake!. Wako sawa sawa kabisa!.
Vivyo hivyo, hadhi za mawaziri na mawaziri vivuli ndani ya bunge ni sawa kabisa, tofauti pekee ni mawaziri wana means zaidi kutokana na uwezeshaji kiliko hawa vivuli!. Mfano Waziri Magufuli, akishakagua barabara au kuizindua, waziri kivuli alipaswa aifanyie ukaguzi na kutoa mawazo yake kama ni chini ya kiwango etc, etc.
Haki zote za Waziri Mkuu bungeni ndizo pia haki za KUB!. 
Japo haijaandikwa kwenye kanuni yoyote kuwa Waziri Mkuu akisimama, "ni lazima spika ampe ruhusa ya kusikilizwa" no matter what!. Spika hana mamlaka yoyote ya kuamua kutomsikiliza Waziri Mkuu anaposimama kwa hoja yoyote!. Vivyo hivyo, spika au naibu spika, "hana mamlaka!" ya kumzuia KUB kuzungumza!. 
Naomba wale wenye mapenzi mema na nchi hii, hebu tuwe wakweli toka ndani ya nafsi zetu, hivi kweli pale bungeni jana, angesimama Waziri Mkuu, Mhe. Mizengo Pinda, hivi kweli Naibu Spika angemwambia "Kaa Chini?!". Angeendelea kusimama hivi Naibu Spika angewaamuru askari wa bunge kumtoa nje?!.
Hadhi ya KUB ni sawa kabisa na Waziri Mkuu, kitendo cha Naibu Spika kumzuia KUB asizungumze, kumuamuru akae chini na kisha kuamuru atolewe nje, "that was provocation kwa wapinzani wote wa kweli!", kiliwatia hasira, na kilichofuata ni actions in provocation!. Chanzo ni ukosefu wa busara ndogo tuu wa Naibu Spika!.
Laiti Mhe. Naibu Spika, angelimruhusu KUB kuzungumza na kuisikiliza hoja yake!, naamini 100% kwa 100%, yote yaliyofuatia yasingetokea!.
Bungu letu lina mapungufu makubwa na ya msingi ya kikanuni za uendeshaji mabunge ya vyama vingi!. Kiukweli kila kunapotokea vurugu bungeni, mimi huwa namkumbuka sana Mhe. Samuel Sitta!.
Kiukweli huko nyuma nimewahi kulalamikia sana uendeshaji wa bunge wa Madam Spika, Mhe. Anna Makinda, lakini sasa sasa nakiri, pamoja na mapungufu yake yote ya kibinaadamu, Mhe. Anna Makinda is better of 100 times than Mhe. Job Ndugai!. This man is a disaster!. 
Wabunge tumieni kanuni namba 135-(1) Kutuondolea mtu huyu, japo najua wabunge wa CCM watautumia wingi wao vibaya kutoipitisha hoja hiyo, ile tuu process ya "kukataliwa!" ni funzo tosha!.
Mwaka mmoja uliopita nilitoa angalizo hili, na leo nalitoa tena! Wito: Wabunge Badilini Kanuni Kuondoa Udikteta wa Spika/N.Spika!

Wasalaam.
Pasco.

Chanzo : JamiiForums

No comments:

Post a Comment