STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Saturday, October 5, 2013

Golden Bush Fc yapanda daraja

Golden Bush iliyopanda Daraja hadi la Tatu Kinondoni
TIMU ya soka ya Golden Bush Fc iliyokuwa ikishiriki Ligi Daraja la Nne Wilayani Kinondoni, imefanikuwa kupanda daraja hadi la Tatu.
Golden Bush klabu mpya katika na iliyokuwa ikishiriki ligi hiyo kwa mara ya kwanza imefuzu daraja la tatu kutokana na kufanya vyema katika mechi zake za mzunguko wa pili. 
Kwa mujibu wa taarifa ya uongozi wa klabu hiyo ni kwamba Chama cha Soka wilayani humo (KIFA) imeitangaza klabu hiyo kupanda daraja.
MICHARAZO inawapa pongezi vijana hao kwa mafanikio hayo na ikiwakumbusha hawapaswi kuvimba kichwa badala yake ijipange kukabiliana na michuano iliyopo mbele yao;
Taarifa hiyo ya uongozi wa Golden Bush unasomeka hapo chini kama ifuatavyo, l 

Wadau,
 
Nimekuwa kimya kwa muda mrefu hii inatokana na majukumu kuingiliana kidogo na kukosa muda wa kuwalisha taarifa mpyampya. Leo napenda niwataarifu kwamba ile timu yetu ya vijana imetangazwa rasmi na KIFA kwamba imepanda daraja la tatu. Hii imetokana na kumaliza mzunguko wa mwisho bila kutoteza mechi hata moja. mimi binafsi nilibahatika kuangalia mechi kama tatu hivi vijana wakifanya mamabo mazito, hakika mpira ni maandalizi na siyo kununua refa. Tumecheza games zote bila kumpa hata shilingi 500 refa nab ado tumefanilkiwa kumaliza ligi katika mzunguko wa pili ambao ni mgumu kabisa bila kufungwa.
 
Binafsi nawapongeza sana vijana kwa kazi kubwa sana lakini pongezi za pekee wanastahili bench la ufundi  chini ya Madaraka Selemani, Katina Shijja na Waziri Mahadhi kwa matokeo mazuri na kupandisha timu daraja ambayo kwa sasa hivi imekuwa gumzo hapa Dar es Salaam. Aidha ningependa kuwopongeza kwana namna ya pekee kabisa wachezaji wa timu yetu ya Veterans kwa msaada mkubwa wa kiushauri kwa mudawao wa kujitolea kutoa mawazo ya kila aina ambayo kwa hakika ndiyo yametufanya tufika hapoa tulipo leo. Nakumbuka hatua ya kwanza kabisa tulifungwa game ya kwanza 1-0, baada ya kupata matokeo yale wazee waliwaita vijana na kuwapa ushauri wa kisaikolojia, kiufundi na kuwaandaa kitalaam kabisa kwa game iliyofuata, nakumbuka tulishinda mecho zote zilizofuata na kuna timu ilikimbia baada ya kuona hadi half time tumewapiga 7-0. Nawashukuru sana watu wazima wakiongozwa na Macocha kwa kazi nzuri nzuri nzuri sana. Ni furaha kubwa nay a pekee unapokuwa na timu inayoandaliwa kucheza mpira siyo kwenda kuloga na kuhonga marefa. Tumefanya kazi yetu na wote kwa pamoja tunastahili sifa na kujipongeza.
 
Golden bush oyeeeeeeeeee!

No comments:

Post a Comment