STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Saturday, October 5, 2013

Kiemba, Niyonzima hapatoshi tuzo za Mwanaspoti Bora 2013


Mkuu wa kitengo cha Uhusiano na Mawasiliano wa Vodacom Tanzania, Joseline Kamuhanda(kushoto)akisaini mkataba wa udhamini wa Tuzo ya Mwanaspoti bora wa soka wa Vodacom 2013,wanaoshuhudia ni Meneja Masoko wa MCL Bernad Mukasa (katikati) na Ofisa Udhamini na Matukio wa kampuni hiyo Ibrahim Kaude.

Meneja Masoko wa MCL Bernad Mukasa(katikati)akizungumza na waandishi wa habari hawapo pichani wakati wa kutangaza mdhamini mkuu wa Tuzo za Mwanaspoti bora wa soka wa Vodacom 2013,Kushoto ni Mkuu wa kitengo cha Uhusiano na Mawasiliano wa Vodacom Tanzania, Joseline Kamuhanda na kulia ni Ofisa Udhamini na Matukio wa Vodacom Tanzania Ibrahim Kaude.
Mkuu wa kitengo cha Uhusiano na Mawasiliano wa Vodacom Tanzania, Joseline Kamuhanda,akiongea na waandishi wa habari (hawapo pichani) wakati wa kusaini mkataba na kutangaza udhamini wa kampuni yake kwa Tuzo za Mwanaspoti bora wa soka wa Vodacom 2013.
 =======
KATIKA kuhakikisha zinathamini na kuleta ladha na ubora wa mchango wa wanasoka nchini wadau wa mchezo wa soka; Mdhamini mkuu wa  ligi ya Tanzania bara Kampuni ya mawasiliano ya Vodacom Tanzania na kampuni ya  Mwananchi Communications Limited (MCL)wameungana katika kuwezesha zoezi la utoaji wa Tuzo ya Mchezaji bora wa soka kwa mwaka 2013.

Tuzo hiyo itashuhudia wachezaji walioingia hatua ya Tano bora, AMRI KIEMBA, HARUNA NIYONZIMA, SHOMARI KAPOMBE, THEMI FELIX, na KELVIN YONDANI wakichuana kuwania umwamba wa soka nchini Tanzania, Baada ya kupigiwa kura na mashabiki na Kamati maalum chini ya Mwenyekiti wake Zamoyoni Mogela kuchambua majina hayo kulingana na kura walizopata.

Akizungumza katika Mkutano wa kutambulisha tuzo hizo Mkuu wa kitengo cha Uhusiano na Mawasiliano wa Vodacom Tanzania, Joseline Kamuhanda, amesema daima Vodacom imekuwa msitari wa mbele katika kuunga mkono michezo nchini, hususani mchezo wa soka na kuhakikisha unakuwa moja ya ajira muhimu kwa watanzania.

"Vodacom tumeendelea kuwa nguzo muhimu katika maendeleo ya soka la Tanzania, sasa soka limekuwa zaidi ya burudani kwa watanzania kutokana na chachu ambayo tumeiweka tangu tuanze kudhamini ligi kuu, ambayo sasa imekuwa na ushindani mkuba na thamani yake inazididi kupanda siku hadi siku" alisema Kamuhanda na kuongeza,

"Mafanikio haya yanayopatikana katika soka letu, yanatokana na nguvu na kujitoa kwa hali na mali, lakini watu wa kwanza ambao wanaleta mafanikio haya ni wachezaji ambao wamekuwa wanapambana kufa na kupona kutoa burudani kwa Watanzania, Ni lazima tuwaenzi wachezaji hawa, Tunapouzungumzia mchezo wa soka tunazungumzia maisha ya watu sasa, Mpira ni maisha ya watu kwani umetoa ajira kubwa kwa jamii ya Watanzania" alisema.

Kamuhanda aliongeza kuwa wameamua kudhamini tuzo hizo ili kuendelea kuwa sehemu ya mafanikio ya soka Tanzania na kuleta mapinduzi katika soka la Tanzania kwa kutambua michango wa wachezaji mbalimbali ambao mpira kwao ndo ajira kuu.

Kwa upande wake Meneja Masoko wa MCL Bernad Mukasa amesema kuwa, waliamua kuanzisha tuzo hizo ili kuendelea kuunga mkono jitihada za wachezaji wa Tanzania na kuleta ushindani na kujenga moyo miongoni mwa wachezaji wa soka nchini.

"Tuzo hizi zinatambulika rasmi kwa jina la zitaitwa MWANASPOTI BORA WA SOKA WA VODACOM 2013. Ni za kipekee na za kwanza kabisa nchini kwa wigo wa wachezaji wanaohusishwa, ushirikishwaji wa uteuzi wa mshindi, na vigezo husika." ALISEMA Mukasa na kuongeza.

"Kwa mwaka huu, licha ya kumpata Mwanaspoti Bora wa soka wa mwaka wa jumla, tuzo hizi zitakuwa na "categories" zaidi ya 10 ikiwemo kocha bora, mwamuzi bora, mchezaji bora wa kike, mchezaji bora chipukizi, "1st eleven", goli bora, mchezaji bora wa kigeni, Mchezi bora wa kulipwa anayecheza nje, na Kipengele kingine kitajulikana siku ya kilele (surprise)." Alisema Mukasa.

Mukasa alihitimisha kwa kusema kuwa ili kuweka usawa miongoni mwa wapenzi wa soka wachezaji hao walioingia katika Tano bora wanaweza kupigiwa kura na Mashabiki kwa  kuandika ujumbe mfupi unaoanza na neno KURA kisha jina la mchezaji anayemchagua kati ya hao waliotajwa na kisha kutuma kwenda namba 15678. Mshindi wa Tuzo hiyo atatangazwa siku ya kilele cha sherehe hizo.
Mwisho 

No comments:

Post a Comment