STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Saturday, October 5, 2013

Simba yabanwa na Ruvu, Tambwe atupia kama kawa

Betram Mwombeki akijaribu kumtoka beki wa Ruvu Shooting (Picha:Francis Dande)
VINARA wa Ligi Kuu Tanzania Bara, Simba jioni hii imeshindwa kuendeleza ubabe wake baada ya kubanwa mbavu na Ruvu Shooting na kutoka sare ya bao 1-1, huku Amisi Tambwe akiendelea kufunga.
Simba ililazimika kusubiri hadi kipindi cha pili kuchomoa bao kupitia mkwaju wa penati iliyofungwa na Mrundi Amisi Tambwe likiwa bao lake la nane.
Ruvu Shooting walitangulia kupata bao lao dakika ya nane tu tangu kuanza kwa pambano hilo lililochezwa kwenye uwanja wa Taifa, Dar es Salaam.
Bao la maafande hao waliokuwa wenyeji wa pambano hilo liliwekwa kimiani na Said Dilunga na kudumu hadi kipindi cha kwanza kilipomalizika.
Hata hivyo kipindi cha pili kilipoanza iliwachukua dakika sita tu Simba kulirejesha bao hilo baada ya Betram Mwombeki kuangushwa langoni mwa Ruvu na mwamuzi kuamuru ipigwe penati iliyolalamikiwa na wachezaji wa maafande hao.
Hata hivyo kwa kuwa uamuzi wa refa ni wa mwisho wachezaji wa Ruvu kwa shingo upande walikubali mkwaju huo upigwe na Tambwe kusawazisha.

No comments:

Post a Comment