STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Wednesday, January 29, 2014

Athuman Idd 'Chuji' arejeshwa kikosini Yanga

Athuman Idd 'Chuji' aliyerejeshwa kikosini Yanga

KIUNGO mkabaji wa timu ya Young Africans Athuman Idd Athuman "Chuji" amerejeshwa kundini kuungana na wachezaji wenzake baada ya awali kuwa amesimamishwa na uongozi kutona na kitendo cha utovu wa nidhamu aliouonyesha mwishoni mwa mwaka jana.
Athuman Idd "Chuji" alisimamishwa na uongozi na Young Africans baada ya kuonyesha utovu wa nidhamu na kuamua kuondoka vyumbani kuelekea nyumbani kabla ya mchezo kumalizika kitu ambacho alikiri ni makosa mbele ya uongozi.
Kwa mujibu wa mtandao wa klabu hiyo ni kwamba uongozi wa Young Africans ulifikia kumpa barua ya kumsimamisha Chuji ambaye alikiri kufanya kosa hilo na kisha kukiri mbele na kuandika barua ya kuomba msamaha na kuahidi kutorudia tena kitendo hicho au kufanya kitendo kingine chochote cha utovu wa nidhamu.
Baada ya kuandika barua kwa uongozi kuomba msamaha, Chuji alipewa onyo kali na uongozi na kupewa kipindi cha matazamio ambapo kwa kipindi cha mwezi mmoja ameonekana kubadilika na kurejea katika nidhamu ya hali ya juu ndani na nje ya uwanja. 
Chuji ataungana na kikosi cha Young Africans keshokutwa kitakapo rejea jijini Dar es salaam tayari kwa mikikimikiki ya Ligi Kuu pamoja na mashindinao ya Klabu Bingwa Afrika ambayo yanatarajiwa kuanza mwishoni mwa wiki ijayo kwa Young Africans kuanza na timu ya Komoronize ya Visiwa vya Comoro.

No comments:

Post a Comment