STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Wednesday, January 29, 2014

Yanga yashushwa kileleni, Azam yazidi kupaa, Mbeya City yabanwa Mlandizi


MABINGWA watetezi wa Ligi Kuu Tanzania Bara, Yanga a.k.a Wazee wa Uturuki wameshushwa kileleni mwa msimamo wa Ligi Kuu Tanzania Bara baada ya kulazimishwa suluhu na Coastal Union jijini Tanga huku Azam ikipata ushindi mwembamba na kukalia kiti.
Bao pekee lililofungwa na Kipre Tchetche limeiwezesha Azam kufikisha pointi 33 baada ya kupata ushindi mbele ya Rhino Rangers ya Tabora.
Pointi hizo ni moja zaidi ya za Yanga ilitoka suluhu na Coastal katika pambano kali lililochezwa Mkwakwani.
Nayo Mbeya City ilipunguzwa kasi na Ruvu Shooting baada ya kulazimishwa sare ya 1-1 kwenye uwanja wa Mabatini, Mlandizi ikiwa ni pointi ya kwanza kwa kocha Tom Olaba tangu aanze kuinoa Ruvu.
Ruvu walikuwa wa kwanza kupata bao lililofungwa na Jerome Lembeni kabla ya Jeremia John kusawazisha. Mabao yote yakifungwa katika dakika 15 za awali za kipindi cha kwanza.

No comments:

Post a Comment