STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Wednesday, January 29, 2014

Huyu ndiye msanii aliyejinyonga Gesti baada ya kuigiza filamu


 
 Marehemu Victor Peter enzi za uhai wake.
****
MSANII Victor Peter kutoka Bongo Movie amefariki dunia usiku wa juzi kuamkia jana 28/01/2014 kwa kujinyonga katika nyumba ya wageni (guest House) moja iliyotambulika kwa jina la SAFARI JUNIOUR iliyoko maeneo ya Kisosora mkoani Tanga.

Mwili wa marehemu umehifadhiwa katika hospitali ya Bombo mkoani Tanga .

Akizungumza na mwandishi wa habari hizi, mmoja kati ya wasanii walioshirikishwa na marehemu katika filamu yake ya mpya ya mwisho inayokwendakwa jina la Chozi, aliyokuwa akirekodi kabla ya kujinyonga, ambayo hadi sasa  bado haijatoka, Msanii huyo aliyetambulika kwa jina la Koba alisema kuwa 
''Siku moja kabla ya tukio hilo Victor, alifanya nao Shooting ya filamu iliyotambulika kwa jina OUR FAMILY ambayo ilikuwa ndio filamu ya pili ya marehemu Victor tangu ajikite katika tasnia ya filamu Bongo Movie.

Filamu hiyo mhusika mkuu alikuwa ni marehemu Victor na katika filamu  alicheza scene inayohusu msiba wa baba yake aliyefariki na yeye mwenyewe mwisho wa filamu alijinyonga.

Baada ya kumaliza zoezi hilo la kurekodi filamu, marehemu aliondoka na wasanii kadhaa wakaelekea katika ATM iliyo maeneo ya mjini kwa ajili ya kutoa hela ili awalipe wasanii waliohusika katika kazi yake.

Akiwa katika ATM hiyo, mtandao ulikuwa ukisumbua na wakati akisubiri  kusubiria mtandao ukae sawa marehemu Victor alibadilika na kuonekana kama amechanganyikiwa, na baada ya muda ATM ilianza kufanya kazi na  akatoa hela wakaelekea Hospitali ya Ngamiani mkoani Tanga, Kufika Ngamiani daktari akatoa tamko kwamba apelekwe Hospitali kuu Bombo.

Hospitali ya Bombo akapimwa kila kitu na kukutwa mzima asiye na tatizo lolote, ikabidi warudi Gest walikofikia maeneo ya Kisosora, Marehemu akawalipa wasanii wote na kuwauliza kuwa kuna mtu anayemdai? 

Wakamjibu hakuna. Kila msanii akaingia chumbani kwake na kuendelea na ratiba binafsi na marehemu aliingia chumbani kwake.

Asubuhi yakuamkia jumanne 28/01/2014 Wasanii wenzake walimgongea mlango wakaona kimya wakapatwa na wasiwasi ikabidi wamuite mwenye nyumba hiyo ya wageni, ambapo alichukua uamuzi wa kutoa taarifa kwa mwenye kiti wa Serikali za mitaa mwenye kiti akatoa taarifa Polisi, Gari ya Polisi ikatia timu katika eneo la tukio na kuvunja mlango, ambapo walimkuta akiwa tayari ameshafariki dunia mwili ukiwa umening'inia'', alisimulia mmoja kati ya wasanii hao.

 M/mungu ailaze roho ya marehemu mahala pema.

No comments:

Post a Comment