STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Wednesday, January 29, 2014

Arsenal yabanwa, Liverpool ikiua, Mata aibeba Mashetani Wekundu

Arsena wakishangilia bao lao
Manchester United wakishangilia bao la kwanza

Nyota wa Liverpool wakipongezana

WAKATI Arsenal iking'ang'aniwa na 'vibonde' Southampton, huku Liverpool wakitoa kichapo cha aibu kwa wapinzani wao wa jadi, Everton, Juan Mata ameanza kibarua chake vyema kwa Mashetani Wekundu baada ya kuisaidia kupata ushindi wa mabao 2-0 nyumbani dhidi ya Cardiff City.
Arsenal iliyokuwa ugenini imejikuta ikipata sare hiyo ugenini huku ikimpoteza kiungo wake Flamin aliyeoonyeshwa kadi nyekundu na kufanya ishindwe kuwakimbia Manchester City ambayo leo itashuka dimbani na iwapo itashinda itakalia kiti cha uongozi kinachoshikiliwa na The Gunners kwa sasa.
Mathieu Flamini alionyeshwa kadi ya moja kwa moja na kuifanya Arsenal icheze pungufu, huku wenyeji wakitangulia kupata bao la kwanza lililofungwa na Jose Fonte dakika ya 21 bao lilidumu hadi wakati wa mapumziko kabla ya kipindi cha pili kuanza kwa Oliver Giroud kuisawazishia Arsenal bao dakila ya 48.
Santi Cazorla aliipa uongozi vijana wa Arsene Wenger dakika ya 52 kabla ya Adam Lallana kusawazisha dakika mbili baadaye na kuifanya Arsenal iendelee kukaa kileleni ikiwa na pointi 52, moja pungufu na Man City itayocheza na Tottenham Hotspus ugenini.
Katika mechi nyingine za ligi hiyo ya England, Liverpool iliiadhibu Everton kwa kuilaza mabao 4-0 mabao yaliyofungwa na nahodha Steven Gerrard, Daniel Sturridge aliyetupia mawili na jingine na kinara wa mabao  Luis Suarez.
Manchester United ikiwa uwanja wa nyumbani ilipata ushindi wa mabao 2-0 huku nyota wake mpya, Juan Mata aliyesajiliwa kutoka Chelsea akionyesha thamani halisi ya fedha alizonunuliwa kwa kuisaidia timu yake kuwafunika Cardiff City.
Mabao ya Robin van Persie na jingine ya Ashley Young yalitosha kumfariji kocha David Moyes ambaye amekuwa hana amani kwa kipindi kirefu tangu aanze kuinoa timu hiyo akitokea Everton.
Mechi nyingine zilishuhudia Swansea City ikiifunga Fulham kwa mabao 2-0, Crystal Palace wakishinda nyumbani vao 1-0 dhidi ya Hull City na Norwich City na Newcastle United walitoka suluhu ya 0-0.
Ligi hiyo itashuhudiwa ikiendelea tena leo kwa michezo kadhaa ukiwamo wa Spurs dhidi ya Manchester City, Aston Villa itakwaruzana na West Bromwich, huku Sunderland  itaikaribisha Stoke City na Chelsea itaumana na West Ham United.
Msimamo wa Ligi unaonyesha Arsenal wanaoongoza wakiwa na pointi 52 kwa michezo 23, ikifuatiwa na Man City yenye 50 na Chelsea ni ya tatu na pointi zake 49, huku LIverpool ikifuatia na pointi 46 baada ya ushindi wa jana.

No comments:

Post a Comment