STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Wednesday, January 29, 2014

Libya yatangulia fainali za CHAN 2014, Zimbabwe yafa kiume!

Libya vs Zimbabwe
LICHA ya kukomaa kwa muda wa dakika 120 na kulazimisha pambano lao la Nusu Fainali dhidi ya Libya kuingia hatua ya kupigiana penati, Zimbabwe imejikuta ikikwama kufuzu Fainali ya CHAN 2014.
Zimbabwe iliyofuzu  kimiujiza kwenye hatua ya mtoano, ilijikuta ikilala kwa mikwaju 5-4 dhidi ya Libya iliyotangulia kwenye fainali na kusubiri mshindi wa mechi ya nusu fainali ya pili kati ya Nigeria na Ghana.
Pambano hilo la Nigeria na Ghana linalosubiriwa kwa hamu kubwa na mashabiki wa kandanda barani Afrika linatarajiwa kuanza muda mfupi baadaye na timu yoyote ikifanya vema itaunga na Libya kusubiri kupepetana Jumamosi.
Mshindwa katika mechi hiyo atakutana na Zimbabwe mapema siku hiyo ya Jumamosi kucheza pambano la kuwania nafasi ya tatu.
Katika pambano la Zimbabwe na Libya lilikuwa kali na timu zote zilifanya kosa kosa za hapa na pale, huku zikibadilisha wachezaji kwa nia ya kuongeza nguvu vikosi vyao, lakini dakika 90 zilimalizika na hata zile 30 za nyongeza nazo ziliisha patupu ndipo ikafuata hatua ya kupigiana penati.
Kwenye hatua ya penati Libya ilipata penati zake kupitia kwa Elmutasem Abushnaf, Mohamed Al Ghanodi  Abdelrahman Fetori, Mohamed Elgadi na Mohamed Fathi Abdaula, huku Mohamed Mahfudh, Ali Salama
na Motasem Sabbou walikosa penati zao.
Zimbabwe ilipata mikwaju yake kupitia Eric Chipeta, Danisa Phiri, Hardlife Zvirekwi na Patson Jaure, huku Simbarashe Sithole, Peter Moyo, Milton Ncube na Ali Sadiki walikosa penati zao.

No comments:

Post a Comment