STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Wednesday, January 29, 2014

Easy Man ayarudia Mashetani


MSANII anayetajwa kama mfalme wa mchiriku kwa sasa nchini, Is'haka Saleh 'Easy Man' ameurejea upya wimbo wake wa 'Mashetani', huku akijiandaa kuutolea video yake.
Akizungumza na MICHARAZO, staa huyo wa wimbo wa 'Kasoro Wewe' ameurudia wimbo huo baada ya kupewa ushauri kwamba awali haukuwa na kiwango kizuri.
Easy alisema baada ya ushauri huo aliamua kurejea tena katika studio za Natal Records zilizopo Mburahati.
"Nimeamua kuurejea tena wimbo wa 'Mashetani' kuurekodi wimbo huo pale Natal Records chini ya Abba Process. Yaani wacha nijisifie kwa jinsi nilivyoomba, ni bonge la wimbo," Easy alisema.
Easy alisema wimbo huo atauachia rasmi hewani wikiendi hii wakati akianza mchakato wa kufyatua video yake.
"Natarajia kuiachia mwishoni mwa wiki wakati nafanya mchakato wa kurekodi video yake ili kusuuza roho za mashabiki wangu," alisema Easy.
Hata hivyo, Easy hakuweza kubainisha video hiyo ataitoa kupitia kampuni gani, ila alisema itafanywa mapema iwezekanavyo

No comments:

Post a Comment