STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Monday, January 6, 2014

Babi ajitabiria makubwa UiTM

Babi (kati)nakiwa na wachezaji wenzake wa UiTM
KIUNGO wa kimataifa wa Tanzania, Abdi Kassim 'Babi' amesema ameyazoea kwa haraka mazingira ya nchi ya Malaysia alikoenda kucheza soka la kulipwa katika klabu ya UiTM na kudai ana imani atafanya vyema Ligi Kuu ya nchi hiyo ikianza.
Nyota huyo wa zamani wa klabu ya Mlandege, Mtibwa Sugar, Yanga, Azam na KMKM, aliliambia gazeti hili kwamba anashukuru kwa kipindi kifupi tangu atue katika nchi iliyopo Mashariki ya Mbali, ameweza kuzoea mazingira na kuzoeana na wachezaji wenzake wanaojiandaa na msimu mpya wa ligi.
Babi anayefahamika pia kama 'Ballack wa Unguja' alituma picha yake ikimuonyesha akiwa na wachezaji wenzake wa klabu hiyo wakiwa wamepozi baada ya kutokana kufanya mazoezi na kusema tofauti na fikira zake Malaysia kunaonekana kutakuwa kwepesi kwake kuliko ilivyokuwa Vietnam alipocheza soka la kulipwa.
Mchezaji huyo aliwahi kuichezea DT Long ya Vietnam kwa muda wa miezi nane baada ya kujiunga nayo mwaka 2010 akitokea klabu ya Yanga na kurejea nyumbani kujiunga na Azam kwa mkataba wa miaka miwili.
"Kwa hali hii nadhani nitafanya vyema kwa sababu nimeyazoea mazingira kwa kipindi kifupi mno tofauti na nilivyodhani. Bahati nzuri asilimia kubwa ya watu wa hapa ni waislam hivyo hata chakula ni kile nilichozea kula. Kwa sasa tunajifua kwa ajili ya msimu mpya wa ligi utakaoanza Januari 18," alisema Babi.
Babi alijiunga na klabu hiyo kwa mkataba wa mwaka mmoja akitokea KMKM waliomsajili baada ya kuachana na Azam aliyoichezea msimu uliopita kwenye Ligi Kuu Tanzania Bara.

No comments:

Post a Comment