STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Monday, January 6, 2014

TPBO yajivua gamba sakata la Cheka

Cheka (kushoto) alipokuwa akichapana na Phil Williams wa Marekani na kutwaa taji la WBF kabla ya kwenda kulipoteza nchini Russia hivi karibuni
OGANAIZESHENI ya Ngumi za Kulipwa Tanzania (TPBO-Limited) imejivua lawama juu ya kitendo cha bondia Francis Cheka kusafiri kwenda Russia bila maandalizi na kuvuliwa taji lake la dunia la WBF.
Kwa mujibu wa taarifa iliyotolewa na oganaizesheni hiyo kupitia Rais wake, Yasin Abdallah 'Ustaadh', TPBO ilihusika kumsaidia Cheka aliyewafuata kulia ukata kupata nafasi ya kwenda kucheza nje kwa malipo yatakayomnufaisha kw akushirikiaa na PST iliyomsaidia kupata kibali cha safari yake nje ya nchi.
TPBO inasema siyo wao au PST ambao walipaswa kujua maandalizi ya bondia huyo ambaye alidai alikuwa katika hali mbaya kiuchumi zilizoathiri biashara zake kwani jukumu hilo ni la bondia mwenyewe na kocha wake.
Taarifa hiyo inasema baada ya Cheka kuwaomba wamsaidie kwa kushirikiana na PST, walimfanyia mipango ya kwenda Russia kupigana kwa makubaliano ya dau la Dola za Kimarekani 10,000 (sawa na Mil. 16) ikizingatiwa hali yake kifedha haikuwa nzuri pia kuwa na mkata bila fedha hakukuwa na faida kwake.
"Cheka alituarifu mimi na rais wa PST, Emmanuel Mlundwa kwamba anakabiliwa na matatizo makubwa sana ambayo yameathiri kwa kiasi kikubwa biashara zake, hivyo tumsaidie apate pambano ambapo bahati alijitokeza promota toka Kenya, Franklyne Imbenzi kabla ya kuzungumza moja kwa moja na promota wa nchini Russia waliyeafikiana baada ya awali Cheka kumgomea Mkenya," taarifa hiyo inasemeka hivyo.
"Naomba muelewe yote yaliyofanyika kuhusu Francis Cheka tulikuwa tunayajadili kwa pamoja kati ya PST, TPBO na bondia mwenyewe, pia katia ngumi za kulipwa bondia ni kama mfanyabiashara uangalia faida hivyo tusibebeshwe lawama kwa kulipoteza taji lake la Dunia," taarifa hiyo iliongeza.
Tarifa hiyo ilimalizia kwa kusema safari nzima ya kwenda Russia kuanzia kusaini mkataba kupewa visa na kupanda ndege hadi nchini humo na kupanda ulingoni, Cheka alikuwa akifanya kwa hiari yake bila kulazimisha hivyo wadau wa ngumi wasitafute mchawi wakati mhusika amefanya mambo kwa utashi wake.

No comments:

Post a Comment