STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Monday, January 6, 2014

Gwiji Eusebio afariki, aliliwa na wengi

Gwiji Eusebio enzi za uhai wake

Akiwajibika uwanjani enzi za uhai wake

Eusebio akiwa na Ronaldo
LISBON, Ureno
GWIJI wa soka wa Ureno na Klabu ya Benfica, Eusebio amefariki dunia akiwa na umri wa miaka 71.
Akiwa amezaliwa nchini Msumbiji mwaka 1942, Eusebio alipelekwa Ureno na Kocha Mkuu wa Benfica, Bela Guttman, ambaye alimsajili  mchezaji huyo mwaka 1961 baada ya kufunga safari yeye mwenyewe ya kwenda Afrika kumuona akicheza.
Mshambuliaji huyo, aliyepewa jina la 'Lulu Nyeusi', aliibuka kuwa mmoja wa magwiji wakubwa kwa klabu na Taifa la Ureno, akishinda makombe ya Ligi ya Kuu mara 11, makombe ya matano ya ndani na 1962 ubingwa wa Ulaya akiwa na Aguias, pamoja na kuiwezesha Ureno kumaliza washindi wa tatu wa Kombe la Dunia 1966.
Kutokana na kasi yake, nguvu na ufundi, Eusebio alikuwa hazuiliki katika Ligi Kuu ya Ureno na alikuwa na wastani wa kufunga zaidi ya bao moja kwa mechi, 'akitupia' mabao 319 katika mechi 313 za ligi, anabaki kuwa mfungaji bora wa zama zote wa Benfica kwa sasa.
Kipaji chake kilimwezesha kumaliza mfungaji bora nchi Ureno mara sita, kushinda mara mbili tuzo ya Kiatu cha Dhahabu cha Ulaya (1968 na 1973) na kushinda tuzo ya Mwanasoka Bora wa Ulaya 1965 wakati Benfica ikitisha katika soka la Ulaya.
Utawala wa Eusebio haukuishia katika ligi za ndani tu. Aliichezea timu yake ya taifa mechi 61 na kuifungia mabao 41 kwa timu ya Taifa ya Ureno, na inayokumbukwa zaidi ni kumaliza fainali za Kombe la Dunia 1966 akiwa mmoja wa nyota wakubwa wa fainali hizo. Alifunga mabao tisa na kutwaa tuzo ya Kiatu cha Dhahabu cha Mfungaji Bora wa Kombe la Dunia 1966 na pia alifunga bao wakati timu yake ilipowalaza Soviet Union 2-1 na kuwa washindi wa tatu.
Baada ya miaka 15 akiwa Benfica, Eusebio alicheza muda wote uliobaki wa soka lake Amerika Kaskazini, akiwakilisha klabu kadhaa za nchini Mexico na Marekani kabla ya kustaafu 1978.
Mshambuliaji huyo anachukuliwa kuwa mmoja wa wanasoka bora zaidi waliopata kutokea duniani na aliwekwa Na.9 katika tuzo ya Fifa ya 'Mwanasoka Bora wa Karne'. Wapo pia wanaomini Eusebio ndiye alikuwa mwanasoka bora kuliko wote duniani -- zaidi ya Pele na Maradona.
Cristiano Ronaldo alikuwa miongoni mwa waliotuma salamu zao za rambirambi kwa gwiji huyo kupitia akaunti yake ya Twitter: "Daima milele, Eusebio, upumzike kwa amani."
Ripoti nchini Ureno zinadai kwamba alifariki baada ya kupatwa na tatizo la moyo kusimama (cardiac arrest) asubuhi ya jana.
Pamoja na Ronaldo, nyota wengine waliomlilia gwiji huyo kupitia kurasa zao za Twitter na hivi ndivyo walivyoandika:-

Xabi Alonso
RIP Eusebio (1942-2014). Mmoja wa magwiji.

Luís Figo
Mfalme!! Grande perda para todos nos! O mais grande!!

Michael Owen
Huzuni kusikia kwamba Eusebio amefariki dunia. Mabao 733 katika mechi 745 daima itabaki kumtambulisha kama gwiji wa kweli wa soka. R.I.P.

Vincent Kompany
Heshima kwa mtu ambaye ameufanyia makubwa mchezo huu ninaoupenda. Eusebio, mmoja wa magwiji bora wa zama zote, alazwe mahala pema.

Manchester United
Tumehuzunishwa kusikia gwiji wa Benfica, Eusebio amefariki dunia. Alikuwa ni bonge la mchezaji na rafiki wa klabu.

No comments:

Post a Comment