STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Tuesday, January 28, 2014

Wachezaji wasiopimwa Afya kuzuiwa kucheza Ligi Kuu



Na Boniface Wambura SHIRIKISHO la Soka Tanzania (TFF), limesema kwamba kuanzia Machi 1, mwaka huu mchezaji ambaye hatakuwa amefanyiwa vipimo vya afya hataruhusiwa kucheza Ligi Kuu ya Vodacom Tanzania Bara.   Taarifa ya TFF leo imesema kwamba, watatoa kwa madaktari wa klabu za Ligi Kuu fomu maalumu za vipimo kwa wachezaji na kila mchezaji atatakiwa kufanyiwa vipimo vyote kama ambavyo fomu imeelekeza. “Hakuna mchezaji atakayeruhusiwa kuendelea kucheza VPL au kuchezea timu za Taifa kama atakuwa hajafanya vipimo hivyo. Machi 1 mwaka huu ndiyo utakuwa mwisho wa kurejesha fomu za vipimo vya wachezaji,”imesema taarifa hiyo ya TFF chini ya rais wake Jamal Emil Malinzi. Aidha, Madakatri wote wa timu za Ligi Kuu kupitia klabu zao wanatakiwa kuwasilisha vyeti pamoja na wasifu wao (CV) TFF kufikia Februari 8 mwaka huu. TFF imesema wasifu na vyeti hivyo vinatakiwa ili kuwezesha Kamati ya Tiba ya TFF kuandaa mafunzo kwa wataalamu hao wa tiba kwa wachezaji.

No comments:

Post a Comment