STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Tuesday, January 28, 2014

Kitimtim cha Ligi Kuu Bara kutimka kesho

Mbeya City watakaikabili Ruvu Shooting
'Vijana wa Oman' Coastal Union watakaoivaa Yanga kesho Mkwakwani
Yanga watakaokuwa wageni wa Wagosi wa Kaya
Azama watakaokuwa nyumbani Chamazi dhidi ya Mgambo

Ruvu Shooting wataweza kuizuilia Mbeya City Mabatini kesho?
Na Boniface Wambura LIGI Kuu ya Vodacom Tanzania Bara,  itaendelea kesho kwa Coastal Union kuikaribisha Yanga kwenye Uwanja wa Mkwakwani mjini Tanga. Kiingilio katika mechi hiyo ni sh. 5,000 na sh. 15,000. Nayo Ruvu Shooting na Mbeya City zitapambana kwenye Uwanja wa Mabatini uliopo Mlandizi mkoani Pwani kwa viingilio vya sh. 10,000 na sh. 5,000. Uwanja wa Kaitaba mjini Bukoba kutakuwa na mechi kati ya wenyeji Kagera Sugar na Mtibwa Sugar. Viingilio ni sh. 5,000 na sh. 3,000.
Azam itaumana na Rhino Rangers katika Uwanja wa Azam Complex ulioko Chamazi, Mbagala. Viingilio ni sh. 10,000 na sh. 3,000.
Yanga SC ambao ndio mabingwa watetezi, wanaongoza Ligi Kuu kwa pointi zao, 31 wakifuatiwa na Azam Mbeya City zenye 30 kila moja baada ya timu zote kucheza mechi 14.

No comments:

Post a Comment