STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Wednesday, March 5, 2014

Petr Cech hakamatiki Tuzo ya Mchezaji Bora Czech

KIPA wa klabu ya Chelsea ya England, Petr Cech hashikiki katika Tuzo yta Mchezaji Bora wa Mwaka wa Jamhuri ya Czech baada ya kutangazwa tena kuwa mshindi wa mwaka 2013 ikiwa ni mara yake ya sita mfululizo kati ya saba aliyonyakua tuzo hiyo.
Cech (31) ameshinda tuzo hiyo kwa mara ya sita baada ya kupigiwa kura nyingi kutoka kwa wachezaji, makocha, viongozi wa shirikisho la soka na waandishi wa habari.
Kiungo wa Arsenal, Tomas Rosicky ameshika nafasi ya pili wakati mchezaji wa Freiburg, Vladimir Darida akishika ya tatu.
Kipa huyo ndiye tegemeo wa Chelsea inayopigana kunyakua ubingwa kwa msimu huu ikiwa chini na kocha aliyewahi kuipa mafanikio huko nyuma, Jose Mourinho.

No comments:

Post a Comment