STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Wednesday, March 5, 2014

Mourinho 'aizuga' Mancehster City mbio za ubingwa England

Jose Mourhino (kulia) na kocha wa Manchester City Manuel Pellegrini  wakisalimiana enzi wakiwa Hispania
LONDON, England
KOCHA wa Chelsea, Jose Mourinho amesema watakuwa wanabadilisha nafasi za mbio za ubingwa wa Ligi Kuu England na Manchester City kutokana na kikosi hicho cha Manuel Pellegrini kuwa na mechi mkononi.
Miamba hiyo ya Stamford Bridge inaizidi City kwa pointi sita baada ya mwishoni mwa wiki kuibuka na ushindi wa mabao 3-1 dhidi ya Fulham, lakini mabingwa wa Kombe la Ligi (Capital One Cup) wana mechi mbili mkononi na wastani mzuri wa mabao ya kufunga na kufungwa kuliko Chelsea.
Pellegrini anawinda mafanikio makubwa kwa kutwaa makombe matatu baada ya kuiongoza City kushinda 3-1 dhidi ya Sunderland Jumapili kwenye Uwanja wa Wembley na kutwaa ubingwa wa Capital One Cup, jambo ambalo Mourinho anasisitiza kuwa kocha huyo raia wa Chile yupo katika nafasi nzuri ya mbio za ubingwa.
"Ninapenda kuwa na bahati mkononi, na City tu ndiyo yenye bahati mkononi mwake," Mourinho alisema. "Kama nitashinda kila mchezo hadi mwishoni mwa msimu, zote 10 – kama hatutaweza labda hatutakuwa mabingwa.
"Kama [City] itashinda mechi zote 12 ilizo nazo, watakuwa mabingwa. Wana bahati mkononi mwao."

No comments:

Post a Comment