STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Wednesday, March 5, 2014

Wawili waongeza mkataba Arsenal na kumpa ahueni Wenger

350594_heroaBaada ya kupoteza mechi yake iliyopita ya ligi kuu ya England klabu ya Arsenal leo imewapa habari nzuri mashabiki wake baada ya kutangaza wachezaji wao wawili wameongeza mikataba ya kuendelea kuitumikia klabu hiyo.
Nahodha wa timu hiyo Mjerumani Per Mertesacker na kiungo Thomas Rosicky wote wametangazwa kuongeza mikataba yao.
“Tunayo furaha kutangaza kwamba Mertesacker na Rosicky wameongeza mikataba ya kuendelea kuwepo hapa,”  Arsene Wenger aliuambia mtandao rasmi wa klabu hiyo.
“Ni wachezaji wazuri na wenye uzoefu, na wameshaonyesha kila siku kwamba wanaweza kucheza kwenye level ya juu.’ – alimaliza Wenger.
Klabu hiyo hata hivyo haijatoa namba ya miaka kamili ya muda wa mikataba mipya.

No comments:

Post a Comment