
Nahodha wa timu hiyo Mjerumani Per Mertesacker na kiungo Thomas Rosicky wote wametangazwa kuongeza mikataba yao.
“Tunayo furaha kutangaza kwamba Mertesacker na Rosicky wameongeza
mikataba ya kuendelea kuwepo hapa,” Arsene Wenger aliuambia mtandao
rasmi wa klabu hiyo.
“Ni wachezaji wazuri na wenye uzoefu, na wameshaonyesha kila siku
kwamba wanaweza kucheza kwenye level ya juu.’ – alimaliza Wenger.
Klabu hiyo hata hivyo haijatoa namba ya miaka kamili ya muda wa mikataba mipya.
No comments:
Post a Comment