STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Wednesday, April 9, 2014

Mourinho noma aivusha Chelsea nusu fainali

* Real Madrid nayo yafuzu licha ya kipigo ugenini
Winner: Demba Ba celebrates after scoring the goal that sent Chelsea into the semi-finals
Oyooooo! Demba Ba akishangilia bao lake dhidi ya PSG
Mourinho celebrates Porto's win at Old Trafford
Kocha Jose Mourinho akiwa katika furaha ya pekee usiku wa jana
Attack: Welsh winger Gareth Bale drives past Milos Jojic
Bale akijaribu kuipigania Real Madrid
Dejection: Dortmund players react at the end of the game - Lukasz Piszczek and Mats Hummels have their head in their hands
Wachezaji wa Dortmund wakiwa hawaamini kama wameng'oka Ulaya
KOCHA Jose Mourinho wa Chelsea amethibitisha kweli ni Special One kweli baada ya kuyapindua matokeo dhidi ya PSG na kutinga nusu fainali Ligi ya Mabingwa Ualaya kwa faida ya bao la ugenini.
Chelsea iliyokuwa imelala wiki iliyopita kwa mabao 3-1 usiku wa jana ilipata ushindi wa mabao 2-0 na kufanya matokeo kuwa 3-3 na Chelsea kufuzu hatua inayofuata wakiwaacha PSG wakirudi Ufaransa vichwa chini.
Bao la dakika ya 88 lililofungwa na Demba Ba, lilitosha kumpa faraja kubwa Mourinho ambaye aliwashangaza mashabiki kwa kumtoa nyota wake Eden Hazard lakini kumbe alikuwa na maana yake.
Andre Schurrle aliyeingia badala ya Hazard aliifungia Chelsea bao la kuongoza katika dakika ya 32 akimaliza kazi nzuri ya David Luiz na kuwafanya The Blues waliokuwa uwanja wa nyumbani wa Stanford Bridge kwenda mapumziko wakiwa mbele kwa bao 1-0.
PSG iliyomkosa nyota wake, Zlatan Ibrahimovic ilipambana hadi mtokea benchi Demba Ba aliyechukua nafasi ya Frank Lampard alipofunga bao hilo dakika tatu kabla ya mchezo huo kumalizika.
Katika mechi nyingine ya robo fainali, Real Madrid iliungana na Chelsea kutinga Nusu Fainali licha ya kipigo cha mabao 2-0 toka kwa wenyeji wao Borussia Dortmund ya Ujerumani.
Dortmund ikiwa kwenye uwanja wake wa Signal-Iduna-Park mjini Dortmund, ilifunga mabao yake katika kipindi cha kwanza kupitia kwa Marco Reus dakika ya 24 na 37 lakini hayawakusaidia.
Katika mpambano la kwanza mjini Madrid, Wajerumani walilala mabao 3-0 na hivyo kujikuta wakiondoshwa mashindanoni na Real kwa jumla ya mabao 3-2.
Madrid pamoja na kuugulia kipigo, lakini inachekelea kuwatoa nishai wapinzani wao hao waliowang'oa kwenye Nusu Fainali ya michuano ya mwaka jana na kwenda kucheza fainali na Bayern Munich.

No comments:

Post a Comment