STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Saturday, April 12, 2014

NUSU FAINALI ULAYA IKO HIVI

* Chelsea vs Atletico, Real v Bayern
http://www.scaryfootball.com/wp-content/uploads/2014/04/Champions-league-semi-final-draw-real-madrid-bayern-munich-atletico-madrid-chelsea-2014-winner.jpg 
http://img.bleacherreport.net/img/images/photos/002/843/906/a5b49d9267ff1018c37bbe654ea8770f_crop_north.jpg?w=630&h=420&q=75
Mashabiki wanasubiri kuona vita kama hii katika Nusu Fainali ya Ligi ya Ualaya baina ya Atletico Madrid na Chelsea
http://www.fifa.com/mm/photo/tournament/competition/01/27/28/06/1272806_full-lnd.jpg
Nyota hawa Robben na Casillas watakutana kwenye mechi baina ya timu zao za Bayern Munich na Real Madrid
KLABU ya Chelsea imejikuta ikiangukia mikononi mwa Atletico Madrid katika mechi ya Nusu Fainali ya Ligi ya Mabingwa Ulaya.
Droo ya Nusu Fainali iliyofanyika jana imemtupa kocha Jose Mourinho kwa vinara wa La Liga, Atletico Madrid waliyoing'oa Barcelona katika Robo Fainali.
Real Madrid itamenyana na mabingwa watetezi, Bayern Munich katika Nusu Fainali nyingine huku mechi za kwanza zikichezwa Aprili 22 na 23 na marudiano wiki inayofuata.
Ikumbukwe kipa tegemeo wa Atletico Thibaut Courtois mwenye umri wa miaka 21 anachezea timu hiyo kwa mkopo kutoka Chelsea.
Tayari UEFA imetoa ruksa kwa Atletico kumtumia kipa huyo baada ya kushtukia dili lililokuwa likifanywa na Chelsea la kutaka kwanza walipwe fedha kutoa baraka hizo.

No comments:

Post a Comment