STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Saturday, April 12, 2014

Nusu fainali za UEFA Europa League hii hapa

http://theoriginalwinger.com/wp-content/uploads/2014/04/Europa-Draw.jpg

http://news.images.itv.com/image/file/375918/article_img.jpg
Juventus
KLABU za Sevilla na Valencia zote kutokea Hispania zimepangwa pamoja katika pambano la Nusu Fainali ya Ligi Ndogo ya Ulaya (Europa League) huku mabingwa wa Italia Juventus wakitupiwa Benfica ya Ureno kupepetana nao katika hatu hiyo katika droo ilitangazwa jana.
Valencia na Sevilla ambazo zilipindua matokeo yao ya awali walipolazwa ugenini na kushinda nyumbani kwa idadi kubwa ya mabao dhidi ya Porto na Basel zinakutana kwa mara ya kwanza kwenye michuano ya Ulaya.
Mechi za mkondo wa kwanza zitachezwa April 24 na kurudiana Mei Mosi kabla ya timu zitakazofuzu hatua hiyo kuumana kwenye fainali Mei 14 mjini Torino, nchini Italia.
Sevilla waliowahi kutwaa taji hilo mara mbili 2006 na 2007 itaikaribisha mabingwa wa 2004 nyumbani kabla ya kuwafuata wapinzani wao sawa itaklavyokuwa kwa Benfica ambayo haijawahi kunyakua taji hilo itakapoikaribisha Juventus waliotwaa taji hilo mara tatu 1977, 1990 na 1993katika mechi ya mkondo wa kwanza kabla ya kuwafuata Waitalia nyumbani kwao mechi ya marudiano.

No comments:

Post a Comment