STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Sunday, June 15, 2014

Ronaldo awatoa hofu Ureno wakijiandaa kuivaa Ujerumani

Ronaldo alipokuwa akitoka uwanjani kwenye mazoezi
WAKATI nchi yake kesho ikitarajiwa kuwa na kibarua kigumu mbele ya Wajerumani katika mechi yao ya kwanza ya Kombe la Dunia, Mshambuliaji nyota wa Ureno, Cristiano Ronaldo amewatoa hofu mashabiki wa timu yake.
Ronaldo aliviambia vyombo vya habari nchini kwake kuwa majeraha ya goti lake la kushoto yamepona, wakati akifanya mazoezi. 
Zaidi mashabiki wapatao 10,000 walikuwepo kutizama mazoezi hayo ya wazi huko Campinas ambapo kuna wakati mwanamke mmoja alikimbia uwanjani na kujaribu kumfikia Ronaldo na kuzuiwa na walinzi kabla ya kukimbia tena mita 40 na kuwekwa chini na walinzi wengine. 
Ronaldo ambaye alicheza mchezo wa kirafiki ambao Ureno iliitandika Ireland kwa mabao 5-1, alimfuata mwanamke huyo aliwekwa chini ya ulinzi na kuweka saini katika fufala yake kabla ya wachezaji wengine wa Ureno nao kuvua fulana zao na kuwarushia mashabiki hao. 
Ureno itakwaana na Ujerumani katika mchezo wao ufunguzi utakaochezwa kesho Jumatatu na inatarajiwa nyota huyo wa Real Madrid atashuka dimbani kuiongoza nchi yake katika pambano hilo.
Nchi hizo mbili zipo kundi moja na timu za Ghana na Marekani zitakazoumana baadaye usiku wa manane hiyo kesho.

No comments:

Post a Comment