STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Sunday, June 15, 2014

Ivo Mapunda atoa darsa Kombe la Dunia

GOLIKIPA wa klabu ya Simba na timu ya taifa 'Taifa Stars', Ivo Mapunda, amesema wachezaji wa soka nchini wanapaswa kuzitumia fainali za kombe la Dunia zilizoanza juzi nchini Brazil kwa ajili ya kujifunza mambo mablimbali ya soka.
Akizungumza jijini Dar es Salaam, Mapunda, alisema kuwa pamoja na kuwa Tanzania haishiriki kwenye fainali hizo lakini kuna nafasi kwa wachezaji kujifunza kitu kwenye michuano hiyo mikubwa Duniani.
"Hatupo kwenye fainali..., lakini tumepata fulsa ya kutazama fainali hizi kupitia luninga, tunaweza kama wachezaji kujifunza kitu kutoka kwa wenzetu," alisema Mapunda.
Alisema kuwa hata kwa viongozi wa soka nchini wanapaswa kujipanga na kuhakikisha mikakati thabiti inawekwa ili Tanzania ishiriki kwenye fainali hizo miaka ijayo.
Alisema kuwa Tanzania bado ipo nyuma kisoka ukilinganisha na nchi zinazoshiriki kwenye fainali za Dunia lakini bado ina nafasi ya kufikia kwenye uwezo wa kucheza kombe la Dunia.
"Hata hizo timu zinazoshiriki sasa hivi zilianza chini kabisa kama sisi, ila wenzetu walikuwa na mipango mizuri..., tupo nyuma sana lakini tunaweza," aliongezea kusema Mapunda.
Alisema kuwa kama hakutakuwa na mipango mizuri, Tanzania itaendelea kuwa wafuatiliaji kwenye luninga wa fainali za kombe la Dunia.

No comments:

Post a Comment