STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Sunday, June 15, 2014

Jahazi la timu ya Babi, UiTM lazama Malaysia

JAHAZI la timu ya UiTM ya Malaysia anayoichezea kiungo mshambuliaji wa kimataifa wa Tanzania, Abdi Kassim 'Babi'juzi lilizamishwa baada ya kucharazwa mabao 4-0 na timu ya DRB-Hicom katika mfululizo wa Ligi Kuu ya nchi hiyo.
Kipigo hichio kilichopatikana kwenye uwanja wa ugenini wa Hang Jebat, mjini Melaka imeifanya UiTM ambayo ilianza kuonyesha matumaini kwa kupata ushindi ushindi na sare mfululizo kiasi cha kuchupa toka nafasi za mkiani hadi nafasi ya 8 kusaliwa na pointi zao 20 baada ya mechi 19.
Timu hiyo itashuka dimbani kesho kujaribu bahati yao mbele ya timu kali ya PBAPP katika mfululizo wa ligi hiyo inayoelekea ukingoni kwa sasa.
Babi alisema walizidiwa mchezao na wapinzani wao na wanajipanga kwa mechi ya kesho nyumbani ili kuibuka na ushindi na kusogea nafasi za juu.

No comments:

Post a Comment