STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Sunday, June 15, 2014

Bacary Sagna atua Manchester City kilaini akiikacha Arsenal

KLABU ya Manchester City imetangaza rasmi kumnasa beki Bacary Sagna kwa uhamisho huru kutoka klabu ya Arsenal. 
Beki huyo wa kimataifa wa Ufaransa amejiunga na mabingwa hao wa Ligi Kuu kwa mkataba wa miaka mitatu baada ya kuthibitisha juzi kuwa hataongeza mkataba na Arsenal. 
Mustakabali wa beki huyo kubakia Arsenal umekuwa mashakani kwa kipindi kirefu baada ya kushindikana kufikiwa kwa makubaliano ya mkataba mpya aliokuwa akiutaka mchezaji huyo. 
Sagna mwenye umri wa miaka 31 ameungana na kiungo wa Porto Fernando ambao meneja wa City Manuel Pellegrini alikuwa akiwahitaji katika kipindi cha usajili wa majira ya kiangazi. 
Kuondoka kwa Sagna kunamuacha kocha Arsene Wenger kutafuta mbadala mpya katika nafasi ya beki wa kulia huku mchezaji wa Atletico Madrid JuanFran na nyota wa Toulouse Serge Aurier wakiwa wachezaji wanaotizamiwa kuziba pengo hilo.

No comments:

Post a Comment