STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Tuesday, June 17, 2014

Kalidjo Kitokololo atua Mashujaa Band, uongozi watamba

Mkurugenzi wa Mawasiliano wa Bendi ya Mashujaa Bw. Maximillian Luhanga akizungumza katika mkutano huo wakati alipomtambulisha rapa Kitokololo kushoto kutoka bendi ya FM Academia kulia ni King Dodoo mshauri wa bendi hiyo.
Kitkololo akitangaza rasmi kujiunga na bendi ya Mashujaa leo kulia ni Mkurugenzi wa Mawasiliano Bw. Maximillian Luhanga.
BENDI ya Mashujaa imemchukua rapa, Kalidjo Kitokololo ‘Kuku’ kutoka bendi ya FM Academia na kusaini naye Mkataba wa miaka miwili.
Akizungumza kwenye ukumbi wa Milenium Business Park leo , Kijitonyama, Dar es Salaam Mkurugenzi wa Mawasiliano wa bendi hiyo, Maximillian Luhanga amesema kupatikana kwa Chitokololo ni furaha kubwa kwao. 
“Kalidjo anakuwa rapa wa tatu katika bendi ya Mashujaa , baada ya Saulo John maaurufu Ferguson na Sauti ya Radi, ambao wote ni wakali, kwa marapa hao wote tunaamini bendi yetu itakuwa inatisha sana,” amesema Luhanga. 
Maxmilian Luhanga amesema Kitokololo anaanza kazi mara moja baada ya kusaini mkataba mpya.
Kwa upande wake, Kitokololo mwanamuziki kutoka Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo (DRC) amesema amekuja Tanzania kutafuta maisha na Mashujaa imempa ofa nzuri ndiyo maana amejiunga na bendi hiyo.
Amesema ameondoka vizuri FM Academia akiwa amewaaga vizuri wenzake ambao wameridhia kuondoka kwake.
Kitokololo amesema kwamba amejiunga na Mashujaa akimfuata King Dodo ambaye kimuziki ni baba yake , King Dodoo ndiye aliyemleta nchini kwa mara ya kwanza mwaka 2004.
Mashujaa itamtambulisha rasmi mwanamuziki huyo katika onyesho maalum litakalofanyika ukumbi wa Letasi Lounge Ijumaa wiki hii. Mashujaa pia wanatarajiwa kuwa na ratiba ndefu mara baada ya mfungo mtukufu wa ramadhani ambapo Maximillian Luhanga amewaambia mashabiki wa bendi hiyo nchini kote kukaa mkao wa kula, Kwakuwa bendi hiyo itakuwa na ziara karibu mikoa yote ya Tanzania ili kutoa burudani kwa mashabiki wao.

No comments:

Post a Comment