STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Tuesday, June 17, 2014

Ghana yafa kiume, Nigeria yabanwa na Iran, Ujerumani dah!

Ronaldo alijitahidi mbele ya Ujeruman, lakini jahazi lao lilizama mara 4
Vita ya Nigeria na Iran ilikuwa hivi
Dempsey akishangilia bao lake dhidi ya Ghana
WAKATI Ujerumani ikitoa onyo katika Fainali za Kombe la Dunia kwa kuigagadua Ureno kwa mabao 4-0 timu za Afrika zimeendelea kuchechemea.
Ghana ilijikuta ikifa kiume mbele ya Marekani kwa kucharazwa mabao 2-1, huku wawakilishi Nigeria wakibanwa mbavu na Iran katika mchezo mwingine.
Ujeruman waliopo kundi G waliitoa nishai Ureno ikiwa na nyota wa dunia, Cristiano Ronaldo kwa kuilaza mabao 4-0 huku beki wake 'mapepe' Pepe alilimwa kadi nyekundu.
Mabao ya Thomas Muller aliyefunga 'hat trick' na jingine la Mats Hummels yalitosha kuiangamiza Ureno katika pambano la kwanza la timu hizo lililochezwa saa 1 usiku.
Baadaye saa nne Nigeria ikisakata kandanda murua ilishindwa kupata ushindi mbele ya Iran iliyotumia muda mrefu kupaki basi na kushambulia kwa pamoja.
Manane ya usiku Ghana walikuwa dimbani kukamilisha ratriba ya mechi za kwanza za kundi G kwa kuvana na Marekani na kujikuta wakilazwa mabao 2-1.
Bao la mapema la Clint Dempsey kwenye sekundi ya 31 na jingine la dakika ya 86 kupitia kwa John Brooks yalitosha kuzima ndoto za Ghana kuambulia sare.
Mshambuliaji huyo wa zamani wa Fulham, aliifungia Marekani inayonolewa na kocha Jurgen Klinsmann alifunga bao hilo dakika nne baada ya Ghana kuchomoa bao kupitia kwa Andre Ayew.
Michuano hiyo itaendelea tena leo kwa michezo mitatu, Algeria wataumana na Ubelgiji, huku Brazil wenyeji wa michuano hiyo watacheza mchezo wao wa pili dhidi ya Mexico na Urusi kupepetana na Korea.

No comments:

Post a Comment