STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Tuesday, June 17, 2014

Shaaban Kisiga aibeba Morning Star

Na Adam Fungamwango
KIUNGO mchezeshaji wa Mtibwa Sugar Shaabani Kisiga, juzi aliipeleka robo fainali ya Wadau Cup timu yake ya Morning Star ya Kiwalani alipofunga bao moja na kutengeneza lingine, ilipoifunga Mwananyamala Veterani mabao 2-0.
Mechi hiyo kali ilifanyika kwenye uwanja wa shule ya msingi Mwananyamala ambako michuano hiyo inafanyika.
Kisiga ambaye pia ni mchezaji wa zamani wa Simba na SC Villa ya Uganda, alifunga bao kwenye dakika ya 75 kwa shuti kali baada ya kupokea pasi safi kutoka kwa Zokora Nyambiso.
Bao hilo liliamsha mayowe kutoka kwa mashabiki wa timu hiyo baada ya kulisubiri kwa muda mrefu, kwani timu yao ilihitaji ushindi tu ili iweze kusonga mbele.
Mshambuliaji wa Ruvu Shooting Paul Ndauka aliikosesha bao Morning Star katika dakika ya 80 baada ya kupiga shuti lililopaa akibaki yeye na kipa Hamza Zongera wa Mwananyamala Veterani.
Kisiga akiwa katikati ya uwanja alitoa pasi ndefu kwa Nyeje Mussa ambaye hakufanya makosa na kuukwamisha mpira wavuni kwenye dakika ya 88, akiihakikishia timu yake ushindi.
Mbali na Morning Star, timu nyingine zilizofanikiwa kutinga hatua ya robo fainali ya michuano hiyo ni Mbogamboga FC, Sharobaro FC na African People zote za Mwananyamala, Kijitonyama Chipukizi, Generation ya Kinondoni.

No comments:

Post a Comment