STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Tuesday, June 17, 2014

Riyana, Slim wapiga mzigo Zenji


STAA wa filamu nchini, Riyama Ally na Slim Omary 'Kiwi' wapo Zanzibar kwa ajili ya kutengeneza filamu iitwayo 'Dhana' wakishirikiana na wasanii wa visiwani humo.
Akizungumza na MICHARAZO juzi, Kiwi alisema sehemu kubwa ya filamu hiyo imekamilika na walikuwa njiani kurejea jijini Dar es Salaam kuendelea na majukumu yao mengine.
Kiwi alisema mbali na yeye na Riyama filamu hiyo imechezwa pia na msanii maarufu visiwani humo aitwaye Eddy na wakali wengine za Zanzibar na ni 'bonge' la mseto.
"Tupo visiwani kumaliza kushiriki filamu mpya iliyozalishwa visiwani humu iitwayo 'Dhana' ni bonge la filamu kwani kisa chake kina mafunzo makubwa kwa jamii," alisema.
Kiwi alisema simulizi ya filamu hiyo linamhusu mtu mmoja ambaye anamjengea dhana mbaya mkewe kumfanyia usaliti na kuamua kulipa kisasi ambacho kinakuwa majutoa kwake.
"Hii siyo ya kuikosa kwa sababu mikasa kama hii imekuwa ikizikumba nyumba nyingi na watu kuwekeana kinyongo kwa dhana tu, bila ya uhakika wa jambo analodhania," alisema.
Msanii huyo anayetamba

No comments:

Post a Comment