STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Tuesday, June 17, 2014

Ruvu Star kusambaza Spirit videoni

Rogert Hegga
BENDI ya Ruvu Star imekamilisha kurekodi video zao mbili za nyimbo za 'Spirit' na 'Jua Kali' na wanatarjiwa kuanza kusambaza wiki hii ili kuwapa burudani mashabiki wa muziki wa dansi nchini.
Nyimbo hizo zilizorekodiwa video hizo ni kati ya tatu zinazoendelea kutamba kwenye vituo vya redio, wimbo mwingine ukifahamika kwa jina la 'Network Love' ambao video yake imewekwa kiporo kwa sasa.
Akizungumza na MICHARAZO mmoja wa viongozi wa Ruvu, Roger Hegga alisema nyimbo hizo zitasambazwa kuanzia kesho kabla ya bendi yao kuingia tena studio kumaliza kurekodi nyimbo tatu za mwisho za kukamilisha albamu yao ya kwanza.
Hegga alisema walipanga kuingia studio wiki hii, lakini wamesitisha zoezi hilo kupisha maandalizi ya onyesho maalum la 'Usiku wa Mwana Dar es Salaam' litakalofanyika siku ya Jumamosi, jijini Dar.
"Baadhi ya wanamuziki wa Ruvu ni wale walioshiriki albamu ya Mwana Dar es Salaam ya African Stars 'Twanga Pepeta'. hivyo kwa sasa wanamuziki hao tupo katika mazoezi ya onyesho hilo," alisema.
Alisema baada ya onyesho hilo la 'Usiku wa Mwana Dar es Salaam' wanamuziki wa Ruvu watarejea kwenye bendi yao na kufanya mazoezi ya mwisho kabla ya kuingia studio kurekodi nyimbo hizo.
Hegga, mtunzi na muimbaji nyota nchini alizitaja nyimbo hizo za mwisho za kukamilisha albamu yao ni 'Koo' uliotungwa na Khamis Kanyumbu 'Amigolas', 'Chewa Original'-Suleiman Muhumba na 'Facebook' cha mpapasa kinanda Victor Mkambi.

No comments:

Post a Comment