STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Thursday, September 4, 2014

Aisha Bui atupa Mshale wa Kifo mtaani

https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEia3UxHjhFQAOtMelt-HNeHnCq8_8wf46ChclxFiV2yd_QvEl8doJA8VY0-uwmtjMvo2485UzpHaf1mBS6BXhx2VtKIuhIJGQ7MOGFqX5s0a2QX8Qz0bozYXluvp6KZ6mcuSwwpQhDKvLI2/s1600/20+MSHALE+WA+KIFO.jpeg
https://lh4.googleusercontent.com/-DYmmzqm_7HU/U_R5bP2TcCI/AAAAAAAAGoQ/Wy885VogXTc/1.jpeg
FILAMU mpya ya mwanadada Aisha Bui iitwayo 'Mshale wa Kifo' imeachiwa rasmi huku muigizaji huiyo akijipanga kwa ajili ya kutengeneza kazi nyingine mpya.
Akizungumza na MICHARAZO, Aisha Bui alisema filamu hiyo inatoka leo na kwa sasa yeye na 'crew' yake ya Bad Girl 'Film's wapo katika matayarisho wa kuandaa kazi mpya ili kuendelea kuwapa burudani mashabiki wao.
Filamu hiyo ya Mshale wa Kifo ni ya kwanza kiwa mwanadada huyo anayetamba na filamu mbalimbali na ndani ya kazi hiyo ameigiza yeye mwenyewe, Ahmed Olotu 'Mzee Chillo', Salim Ahmed 'Gabo' na wengine.
"Ile filamu ya 'Mshale wa Kifo' imetoka leo baada ya kukwama Agosti 25, kwa sasa Bad Girl Film's tunaanza maandalizi ya kuandaa kazi nyingine mpya, tunataka kuwapa burudani mashabiki wetu mwanzo mwisho sambamba na kuleta mapinduzi ya kuondokana na filamu za 'sebuleni' na ufukweni," alisema Aisha Bui mama wa mtoto mmoja.
Kabla ya kutoa filamu hiyo mwanadada huyo, alitamba na filamu kama Saturday Morning, Better Days, Not Without My Son, Continous Love, Revenge of Love, Mirathi, Pain of Love, Crazy Love na The Second Wife.








No comments:

Post a Comment