STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Tuesday, September 23, 2014

Rooney, Gerrard wapigwa 'madongo' England

http://www1.pictures.zimbio.com/gi/Wayne+Rooney+Steven+Gerrard+England+v+Ukraine+ygx0xe1DQpXl.jpg

MWANZO mbaya wa msimu kwa klabu za Manchester United na Liverpool unachangiwa na manahodha wao wawili Wayne Rooney na Steven Gerrard, imeelezwa.
Mchambuzi wa soka wa Goal.com, Greg Stobart, amesema "upendeleo" wanaopata Rooney na Gerrard kwa kuwa manahodha na kuachwa waendelee kubaki uwanjani licha ya kucheza chini ya kiwango, kunazigharimu timu hizo hasa katika zama hizi ambazo hata nyota wakubwa wa kimataifa huachwa benchi.
Wakati Juan Mata alianzia benchi na Di Maria na Radamel Falcao nao wakamalizia mechi wakiwa benchi, Rooney aliendelea kunufaika kwa "upendeleo" wa kubaki uwanjani kwa dakika 90 zote, licha ya kupiga shuti moja tu langoni mwa Leicester katika kipigo chao cha 5-3 juzi Jumapili.
Kuna maswali yanayohoji kama Rooney anastahil nafasi kikosi pamoja na wakali kama Falcao, Di Maria na Robin van Persie. Tabia yake ya kupooza mpira haiendani na falsafa ya kocha Louis Van Gaal ya soka la kushambulia.
Van Gaal said alisema Ijumaa iliyopita kwamba Rooney, kwa kuwa nahodha, anatarajia kuendea kunufaika na "upendeleo" wa kuanza katika mechi ngingi zaidi msimu huu na kubaki uwanjani kwa muda mrefu zaidi linapokuja suala la kocha kufanya mabadiliko. Jambo hilo linampa uhakika mchezaji ambaye wengi wanaona kwamba hastahili kuanza katika kikosi chenye sura mpya cha Manchester United. Na kipigo cha 5-3 dhidi ya Leicester juzi ni mfano unaoonyesha ni kwa nini.
Alionekana akiwawakia kwa hasira wachezaji wenzake, ikiwamo kumshukia beki yosso Tyler Blackett (20) kufuatia Leicester kufunga goli la 3-3, lakini Rooney alionyesha kutojielewa kwani yeye ndiye aliyepoteza mpira uliozaa goli hilo.

No comments:

Post a Comment