STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Tuesday, September 23, 2014

Fainali za Kombe la Dunia 2022 nchini Qatar zayeyuka

https://www.venturesonsite.com/news/wp-content/uploads/2014/06/qatar-chronicle-qatar-2022-stadiums.jpgIMEBAINIKA wazi kuwa ni ndoto kwa Fainali za Soka za Kombe la Dunia za mwaka 2022 kufanyika Qatar.
Mjumbe wa kamati ya utendaji ya Shirikisho la Soka Duniani,FIFA, Theo Zwanziger amefichua kuwa ni vigumu fainali hizo kuchezwa nchini humo kutokana na hali ya joto kali katika nchi hiyo.
Zwanziger ambaye ni raia wa Ujerumani aliliambia jarida la michezo la Bild jana kuwa anadhani mwisho wa siku michuano ya Kombe la Dunia 2022 haitafanyika katika nchi hiyo. 
Mjumbe huypo aliendelea kudai kuwa watabibu wamesema hawatakubalia kuwajibika kama michuano hiyo itafanyika katika hali ya hatari kama hiyo. 
Japo Qatar wamesisitiza ambao ni matajiri wakubwa wa mafuta wamesisitiza kuwa wanaweza kuandaa michuano hiyo majira ya kiangazi kwa kutumia teknolojia ya vipoza hewa katika viwanja vyake, sehemu za mazoezi na mahali watakapofikia mashabiki bado kumekuwa na wasiwasi mkubwa kuhusiana na afya za wachezaji na mashabiki watakaokuja kushuhudia michuano hiyo. 
Zwanziger amesema anajua wanaweza kuweka vipoza hewa viwanjani lakini Kombe la Dunia halichezwi viwanjani pekee kwani mashabiki kutoka duniani kote watakwenda na kusafiri katika hali hiyo ya joto jambo ambalo ni hatari kwa afya na maisha yao. Michuano ya mwaka 2022 imekuwa ikileta mjadala mkubwa huku rais wa FIFA Sepp Blatter akikiri kuwa walifanya makosa kuipa Qatar kuandaa michuano hiyo na kutaka kuangalia uwezekano wa kuamisha michuano hiyo ichezwe katika majira ya baridi.

No comments:

Post a Comment