Mechi hiyo itapigwa kwenye Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam ambapo awali ilielezwa kuwa Simba ingecheza na Mtibwa Sugar kabla ya kuwepo kwa mabadiliko hayo. Taarifa toka ndani ya Simba zimesema maandalizi ya mechi hiyo yanaendelea vizuri, timu ikiwa kambini Zanzibar, chini ya Kocha wake mzoefu, Patrick Phiri kutoka Zambia. Kwa mujibu wa habari hizo, Simba huenda ikacheza mechi nyingine ya kirafiki ya kimataifa wiki ijayo kwa kumenyana na APR ya Rwanda. Mechi dhidi ya Gor Mahia itapigwa Jumamosi wakati mechi dhidi ya APR itapigwa Jumatano ijayo kwenye uwanja huo na ni maelekezo ya kocha Phiri.
STRIKA

USILIKOSE

Wednesday, September 3, 2014
Simba kuivaa Gor Mahia, APR Rwanda Dar
Mechi hiyo itapigwa kwenye Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam ambapo awali ilielezwa kuwa Simba ingecheza na Mtibwa Sugar kabla ya kuwepo kwa mabadiliko hayo. Taarifa toka ndani ya Simba zimesema maandalizi ya mechi hiyo yanaendelea vizuri, timu ikiwa kambini Zanzibar, chini ya Kocha wake mzoefu, Patrick Phiri kutoka Zambia. Kwa mujibu wa habari hizo, Simba huenda ikacheza mechi nyingine ya kirafiki ya kimataifa wiki ijayo kwa kumenyana na APR ya Rwanda. Mechi dhidi ya Gor Mahia itapigwa Jumamosi wakati mechi dhidi ya APR itapigwa Jumatano ijayo kwenye uwanja huo na ni maelekezo ya kocha Phiri.
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
No comments:
Post a Comment