STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Sunday, September 21, 2014

Simba yashindwa kulipa kisasi kwa Coastal Taifa

simba
MASHABIKI wa klabu ya Simba wametoka uwanja wa Taifa wakiwa hawana furaha baada ya kikosi cha timu yao kushindwa kulinda mabao mawili waliyoyafunga kipindi cha kwanza na kuwaachia Coastal Union warejeshe kipindi cha pili na kufanya mchezo huo kumalizika kwa sare ya mabao 2-2 katika Ligi Kuu.
Mabao mawili ya Shaaban Kisiga na Amissi Tambwe yaliwafanya vijana wa Msimbazi kuwa na furaha na kuamini wangepata nafasi ya kuwacheka wapinzani wao Yanga waliozabuliwa mabao 2-0 na Mtibwa Sugar jana mjini Morogoro baada ya kwenda mapumziko wakiwa mbele.
Hata hivyo kipindi cha pili kilipoanza Coastal waliingia kivingine na kucharuka na kurejesha bao moja baada ya jingine kupitia wa Lutimba Yayo na Ramadhani Salim kufungwa kwa faulo na kuifanya matokeo kusomeka mabao 2-2 na kuwafanya mashabiki wa Simba kuwa wanyonge, licha ya timu ya kupata pointi moja.
MSIMAMO LIGI KUU TANZANIA BARA 2014-2015
                                          P  W  D  L  F  A  Pts
1. Ndanda Fc                    1   1    0   0  4   1    3
2. Azam                             1   1    0   0  3   1   3
3. Mtibwa Sugar                1   1    0   0  2    0  3
4. Prisons                           1   1   0   0   2   0   3
5. Mgambo JKT                1    1   0   0   1   0   3
6. JKT Ruvu                      1    0   1   0   0   0   1
7. Coastal Union                1    0   1   0   2   2   1
8. Simba                            1    0   1   0   2   2   1
9.Mbeya City                     1    0   1    0   0  0  1
10. Kagera Sugar               1    0   0   1    0   1   0
11. Ruvu Shooting              1    0   0   1    0   2  0
12.Yanga                            1    0   0   1    0   2  0
13. Polisi Moro                  1    0   0   1    1    3  0
14.Stand Utd                     1    0   0   1    1    4  0

No comments:

Post a Comment