STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Sunday, September 21, 2014

TP Mazembe yafa ugenini kwa ES Setif

http://www.groupelavenir.org/IMG/arton1718.jpg
TP Mazembe
KLABU ya TP Mazembe ya DR Congo imepewa kipigo cha mabao 2-1 ugenini na ES Setif ya Algeria, lakini bao la kujifunga ,a wenyeji limewasaidia kuwaweka katika nafasi nzuri ya kusonga mbele kama itashinda angalao bao 1-o nyumbani wiki ijayo.
Said Aroussi alijifunga kattika dakika 52 kwenye harakati za kuokoa mpira wa krosi uliopigwa na Rainford Kalaba na kuwapa uongozi TP Mazembe.
Hata hivyo wenyeji walirudisha bao hilo dakika chache baadaye kupitia kwa Younes akimalizia krosi pasi huku waamuzi wa poambano hilo wakijichanganya, refga wa kati akisema goli wakati msaidizi wake akionyesha kibendera cha kuotea cha mpiga krosi.
Refa Neant Alioum alikubali goli hilo baada ya kuzongwa na wachezaji wa ES Setif wakipinga maamuzi ya mshika kibendera, japo TP Mazembe waliamua kucheza soka.
Dakika chache kabla ya kumalizika kwa pambano hilo wenyeji walipata bao la ushindi kupitia kwa Abdulmalek Ziaya aliyemtungua kipa mwenye mbwembwe Robert Kidiaba.

No comments:

Post a Comment