STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Thursday, October 23, 2014

Liverpool yafa nyumbani, Ronaldo acha bhana, Arsenal chupuchupu

Cristiano Ronaldo scored the opener for Real Madrid at Liverpool

Cristiano Ronaldo and Mario Balotelli ahead of the Liverpool-Real Madrid game

Cristiano Ronaldo scored the opener for Real Madrid at Liverpool
Ronaldo akifunga bao la kwanza la Real Madrid
Karim Benzema scored twice in the first half for Real Madrid against Liverpool
Benzema akishangilia moja ya mabao yake jana
Mario Balotelli was taken off at half time for Liverpool against Real Madrid
Balotelli akiwa na Pepe
Lukas Podolski
Pongezi zako kaka!
Anderlecht 1-0 Arsenal
Najar akiwatungua Arsenal
CHRISTIANO amemfikia Lionel Messi katika orodha ya wanaokimbilia kuvunja rekodi ya mabao inayoshikiliwa na Raul ya mabao 71 baada ya kuisaidia Real madrid kuinyuka Liverpool 3-0 ikiwa kwao.
Ronaldo alifunga bao la kuongoza dakika ya 23 likiwa ni bao la 69 katika Ligi ya Mabingwa Ulaya kutokana na mechi 105 na kuwa sawa na Messi aliyecheza mechi 88 tu na kusaliwa mabao mawili kumfikia Raul.
Katika pambano hilo lililoshuhudiwa mshambuliaji wa kiitalia, Mario Balotelli akitolewa wkaati wa mapumziko na kubadilishana jezi na beki Pepe Karim Benzema alifunga mabao mawili.
Benzema anayesifiwa na Ronaldo kuwa ndiye namba 9 bora duniani alifunga dakika ya 30 na 41 na kuwazamisha vijana wa Brendan Rodgers aliyenukuliwa hatamvumilia tena Balotelli kwa alichokifanya uwanjani jana.
Katika mechi nyingine ya kundi hilo la B, Ludogorets Razgrad imeichapa bao 1-0 Basel, huku katika mechi nyingine Arsenal ilitakata ugenini baada ya kuilaza Anderlecht mabao 2-1.
Mabao ya 'usiku' ya Kieran Gibbs na mtokea  benchi, Lukas Podolski yaliiokoa Arssenal isizame Brussels, Ubelgiji.
Wenyeji walipata bao dakika ya 72 kupitia Andy Najar kabla ya Gibbs kufunga dakika 88 na Podolski asiye na furaha Emirates kwa sasa kufunga dakika za nyongeza.
Arsene Wenger amedokeza kuwa hawana mpango wa kumuuza Mjerumani huyo mwenye asili ya Poland japo mwenyewe amekuwa akisisitiza kuwa Januari ataondoka Emirates akatafute mahali atakapoaminiwa na kucheza kwa raha zake.

No comments:

Post a Comment