STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Thursday, October 23, 2014

Wolfsburg watakata ugenini Europe League



http://www.uefa.com/MultimediaFiles/Photo/competitions/Comp_Matches/02/15/88/77/2158877_w2.jpg
KLABU ya Wolfsburg ya Ujerumani jioni hii imepata ushindi mnono ugenini baada ya kuibamiza FK Krasnodar ya Russia katika mechi ya Kundi H ya michuano ya Ligi Ndogo ya Ulaya Europe League.
Wageni hao walianza kwa kuzawadiwa bao na beki wa Krasnodar, Andreas Granqvist kujifunga dakika ya 37 bao lililodumu hadi mapumziko.
Washindi hao waliongeza bao la pili kupitia Kelvin De Bruyne dakika ya 46 akimalizia kazi na Naldo kabla ya Granqvist kusahihisha makosa yake kwa kuifungia timu yake bao kswa penati dakika ya 51.
Mshambuliaji Luiz Gustavo aliiongezea Wolfsburg bao la tattu dakika ya 64 kabla ya Bruyne kuongeza jingine dakika ya 79 na wenyeji kupata bao la pili la kufutia machozi lililofungwa na Wanderson katika dakika ya 86.
Mechi nyingine za makundi kwa michuano hiyo ya Ulaya inaendelea usiku huu.

No comments:

Post a Comment